November 12, 2018


Ikiwa ni takribani siku mbili pekee tangu kuteuliwa kwa Thobias Langalanga kuwa Kaimu Mwenyekiti wa klabu ya Yanga, kiongozi huyo ameamua kujivua wadhifa huo jana.

Langalanga ameamua kujivua kutokana na kurejea kwa Yusuf Manji ambaye alitangaza kujizulu takaribani mwaka mmoja na miezi kadhaa sasa imepita.

Kujivua kwa Langalanga ambaye ni Mjumbe wa Kamati ya Utendaji kumemfanya afunguke kuwa yeye anamkubali Manji hivyo hana haja ya kuendelea kushikilia nafasi hiyo.

Kupitia Baraza la Wadhamini Yanga, Mwenyekiti wake, George Mkuchika, alisema Manji ameandika barua ya kuomba kurejea kwenye nafasi yake hivyo hakuna tena haja ya kujaza nafasi ya Uenyekiti.

Kuelekea uchaguzi wa Yanga utakaofanyika January 13 2019, Yanga itafanya uchaguzi wa kujaza nafasi zingine zilizo wazi ikiwemo baadhi ya nafasi za Kamati ya Utendaji, Katibu Mkuu na Makamu Mwenyekiti.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic