November 5, 2018


Wakati dirisha la usajili Tanzania Bara likitarajiwa kufunguliwa Novemba 15, mwaka huu, imebainika kwamba wachezaji mbalimbali wa kimataifa kutoka mataifa mbalimbali ya Afrika wameomba kusajiliwa katika klabu hiyo inayonolewa na Mbelgiji Patrick Aussems.

Wachezaji hao wameomba kusajiliwa Simba kutokana na klabu hiyo kwa sasa kumwaga fedha za usajili kutokana na uwepo wa mwekezaji wake, Mohammed Dewji.

Akizungumza jana kwenye mkutano mkuu wa klabu hiyo, Kaimu Rais aliyemaliza muda wake, Salim Abdallah ‘Try Again’ amesema kwamba wamepokea meseji mbalimbali kutoka kwa wachezaji wa kimataifa wakiomba kusajiliwa katika klabu hiyo.

“Kuna wachezaji mbalimbali ambao wameomba kusajiliwa katika klabu yetu katika kipindi hiki. Nimekuwa nikipokea meseji za wachezaji kutoka sehemu mbalimbali za Afrika wakiomba nafasi ya kusajiliwa ndani ya timu yetu,” alisema Try Again.

Licha ya wachezaji hao kuomba kusajiliwa na Simba klabu hiyo kwa sasa ina wachezaji nane wa kimataifa. Wachezaji hao ni Emmanuel Okwi (Uganda), Claytous Chama (Zambia), Pascal Wawa (Ivory Coast), Meddie Kagere (Rwanda), Nicholaus Gyan (Ghana), Asante Kwasi (Ghana), Juuko Murshid (Uganda) na James Kotei (Ghana).

Wakati huohuo jana Simba walitangaza kutenga kiasi cha milioni 750 kwa ajili ya kufanya usajili kwa ajili ya kukiimarisha kikosi hicho.

Katika hatua nyingine, Try Again amesema kwamba klabu hiyo tayari imekamilika na wanajua watasajili wachezaji gani kwenye dirisha la usajili ambapo usajili huo utasimamiwa na mwekezaji, Mohammed Dewji ‘Mo’.

Pia klabu hiyo imesajili wachezaji 17 kwenye kikosi cha vijana cha klabu hiyo U20 pamoja na kusajili wachezaji 10 wanaocheza kwenye timu ya taifa ya wanawake kwa ajili ya Simba Queens.

1 COMMENTS:

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic