ZAHERA AMTAJA KIBOKO WA SIMBA ALIYEIMALIZA TP MAZEMBE
Kocha Mkuu wa Yanga, Mwinyi Zahera raia wa DR Congo ameweka wazi kwamba anamuamini straika wake, Heritier Makambo kuwa ana uwezo wa kufunga zaidi ya mabao 16 kwenye ligi kutokana na kufunga idadi hiyo kwenye ligi ngumu ya Congo.
Makambo ana mabao saba sambamba na washambuliaji wa Simba, Meddie Kagere na Emmanuel Okwi .
Zahera amesema kwamba anamuamini kwa sababu tayari alishafanya naye kazi nchini Congo na alifunga mabao mengi akipambana na timu kama TP Mazembe, hivyo hawezi kushindwa kufunga katika ligi ya Tanzania kutokana na kutokuwepo ugumu sana kulinganisha na huko.
“Wakati ambao Makambo hakuwa anafunga mashabiki wakaanza kuongea lakini niwaambie kwamba hilo suala siyo ishu kwake kwa sababu nimefanya naye kazi DR Congo aliwahi kufunga mabao 16 kwenye mechi nane za ligi.
“Kwenye suala la kufunga ninamuamini kwamba hataniangusha na niwaambie kwamba atafunga zaidi, ni suala la kupewa muda tu,” alisema Zahera.
Lakini sasa kwa tunavyowajua TP Mazembe kwa kupenda vilivyo bora katika suala la kutafuta wachezaji wenye uwezo vipi washindwe kumuona makambo kama kweli ni mchezaji mwenye uwezo? Na vipi makambo anakubali kushinda na njaa pale yanga wakati hata mtibwa ingempeleka kimataifa na asingeasirika kisaikojia kutokana na migomo ya wachezaji pale yanga. Ligi bado mbichi tena sana kwa hivyo wacha tuone nini kitatokea.
ReplyDeleteNakubaliana na coach kuwa makambo ni mshamuliaji mzuri ukifananisha na wengine kwa kigezo kimoja tu...makambo amejitahidi kufunga magoli yote saba ktk mechi tofauti kila goli lkn wengine wamefunga goli mbili mbili ktk mechi rahisi lkn mikoani wameshindwa kufunga...ligi bado ndefu tutaelewana tu
DeleteNikweli makambo amejidhihirisha kwamba nimshambuliaji mzuri ukiangalia hata aina yamagolianayofunga,napingana nahoja kwamba makambo kama mzuri kwanini asingeenda tp mazembe hiyo nihoja dhaifu sana kwanihata kule Kongo sio kila mchezaji.mzuri anacheza tp mazembe zipo timu nyingi.mzuri.pale kuna As vita,motema pembe.nazo zina mastaa
DeleteNikweli makambo amejidhihirisha kwamba nimshambuliaji mzuri ukiangalia hata aina yayamagolianayofunga,napingana nahoja kwamba makambo kama mzuri kwanini asingeenda tp mazembe hiyo nihoja dhaifu sana kwanihata kule Kongo sio kila mchezaji.mzuri anacheza tp mazembe zipo timu nyingi.mzuri.pale kuna As vita,motema pembe.nazo zina mastaa
DeleteSasa hapo kiboko ya simba ndo nan??? huu ni ujinga wa kiwango cha phd
ReplyDeleteSo mama Zahera haji tena kuichezea Yanga?
ReplyDelete