UMESIKIA huko mtaani kwamba wako wanaodanganyana kwamba kwa kuwa Rais John Pombe Magufuli hayupo tena madarakani, basi fedha zitapatikana kwa wingi.
Wajinga
wengine wanawalaghai wengine lakini wanaolaghaiwa, hakuna hata mmoja anajibu
sahihi kama utamuuliza kwamba fedha hizo zitapatikana vipi bila ya kufanya
kazi.
Wanaofikiria
fedha itapatikana tu kwa kulala ndani wanajidanganya, hata Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan hawezi kutoa nafasi hiyo na mwisho
tutamlaumu tu.
Lazima
kuchapa kazi ili kutafuta maisha yako, lazima kujituma na kupambana kupata kile
kilicho sahihi na si kusubiri ulalamike tu au kuamini kufariki dunia kwa
Magufuli na wepesi wa maisha yako.
Watu wa aina
hii nimeamua kuwazungumzia kidogo kwa kuwa huku mitaani kwetu imekuwa gumzo kwa
watu kuamini eti unafuu wa maisha umewadia. Fanyeni kazi, tuache longolongo.
Zaidi huku
ni nilitaka kama kupita na kukumbushana tu lakini lengo hasa nilikuwa nimeamua
kulenga kuhusiana na nidhamu ya uongozi michezoni ambayo imechangia mambo mengi
makubwa.
Nidhamu hii
ilipatikana wakati wa uongozi wa Hayati Magufuli, unaona karibu kila sehemu kwa
maana ya sehemu mbalimbali kama klabu, mashirikisho au vyama vya michezo, suala
la nidhamu katika uongozi ilikuwa juu.
Popote pale
ambako kunakuwa na nidhamu, lazima kunakuwa na mafanikio na hasa katika suala
la uongozi. Maana viongozi wanakuwa wanafanya vitu vyao kwa weledi, wanafikia
malengo kwa utekelezaji bora unaolindwa na nidhamu ya kiuongozi.
Mwisho wa
nidhamu ya kiuongozi ni kufikia malengo na baadaye kwenda katika mafanikio.
Najua unanielewa kwa kuwa Rais Magufuli hakuwa anaongoza michezo. Lakini aina
yake ya uongozi wa Serikali ya awamu ya tano, ulifanya kila sehemu waige na
kuachana na zile tabia za uzembe, kuamini mashirikisho au vyama vya soka ni
mali yao.
Badala yake,
ile aina ya Magufuli ya utendaji uliotukuka kwa ajili ya wananchi ukasonga na
kufanya vema, wengi wakiiga na mwisho umeona kuwa na mafanikio na mabadiliko
makubwa ya kiuongozi.
Mfano,
Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), limepata mafanikio makubwa katika timu za
taifa kuanzia vijana U17, U20, timu zote za wanawake na hata ile kubwa.
Kushiriki
Afcon kwa mara ya pili halikuwa jambo jepesi lakini Taifa Stars ikarejea tena
Chan, mara ya mwisho ikiwa ni 2009 nchini Ivory Coast. Timu za wanawake za U
20, U17 zikabeba makombe yote Cosafa lakini pia Cecafa. Timu za vijana
zikashiriki michuano mikubwa ya Afcon.
Tuwapongeze
TFF, wamefanya kazi kubwa lakini pamoja na ubora wao lazima wakubali alama za
nyakati zimewaongoza na kufanya haya makubwa ingawa kuna baadhi hawayaoni.
Tunajua
Simba na Yanga wamekuwa wakifanya kazi kwa juhudi kubwa kwao, wanashindana wao
lakini unaiona nidhamu ya uongozi wakijua Serikali ipo macho.
Mawaziri wa
Michezo wamekuwa na nguvu sana katika kipindi cha Rais Magufuli, wamechangia
wale waliokuwa wakifuja mali michezoni, wakifanya mambo kwa kubahatisha kuingia
woga kwa kuwa wanatambua Serikali ipo.
Haya
katuacha Rais Magufuli, hatupaswi kuyabwaga kibarazani halafu baadaye tuanze
kumlaumu Rais Samia kwamba alichangia.
Tunatakiwa
kuendelea kupita njia ileile ili kufanya mambo yaendelee kwenda na tukumbuke
Magufuli ni mzazi au mwalimu. Alichokifundisha, kinatakiwa kuendelezwa na si
inapokuwa hayupo, basi kife. Somo lake lilikuwa linaumiza kwa kuwa watu
walizoea kuishi kwa mazoea lakini ukweli bila kificho umeonekana kwamba
anachokitaka ni kweli na juhudi zake ni kuliongoza taifa kwa ufasaha na
mafanikio na taifa lenyewe ni sisi.
Kama kweli
tunaamini hakuwa mwanamichezo sana lakini kuna masomo alitupa na leo yamesaidia
mabadiliko michezoni, basi sisi ni wanafunzi tulioiva na tunapaswa kufanya
kilicho sahihi kuendeleza michezo.
kwa mfano mkulima wa pamba, anafanya kazi halafu soko la uhakika halipo ,,,kutwa nzima serikali bize na kukusanya ushuru kwa wajasiria mali,,hata kile kidogo tuchopata kinarudi serikalini lini tutainuka ?,,, mlala hoi na ndege wapi na wapi ? mtuletee basi hata madawa kwny vituo vya afya.
ReplyDelete