July 22, 2020



LEO Julai 22 Ligi Kuu Tanzania Bara inaendelea ambapo vita ni kubwa kwenye upande wa kusaka nafasi ya kubaki ndani ya Ligi Kuu Bara.

Timu 10 zitakuwa uwanjani kusaka pointi tatu kwenye viwanja tofauti na hesabu zao zipo namna hii:-

Mbao v Namungo, Uwanja wa Kirumba( Mbao ipo nafasi ya 19 ina pointi 39 inakutana na Namungo ina pointi 64 nafasi ya nne).

Safu ya ushambuliaji ya Mbao imefunga jumla ya mabao 28, kinara ni Wazir Jr ana mabao 12/ Namungo safu yao ya ushambuliaji imefunga mabao 44 kinara wao ni Relliants Lusajo ana mabao 12.

Mbao inasaka nafasi ya kubaki ndani ya Ligi Namungo haina cha kupoteza ila inawania nafasi ya pili kimyakimya.

Singida United v Kagera Sugar, Liti( Singida United ina uhakika wa kushiriki Ligi Daraja la kwanza ina pointi 18 baada ya kucheza mechi 36/ Kagera Sugar wana uhakika wa kubaki ndani ya ligi, ipo nafasi ya 8 pointi 49.

Mwadui v Biashara United, Karume/Fainali ya kusaka nafasi ya kubaki ndani ya ligi,  Mwadui FC ipo nafasi ya 15 pointi 41/ Biashara United nafasi ya 9 pointi 47 ikipoteza mechi mbili inakwenda na maji.

Mtibwa v Yanga, Jamhuri/ Mtibwa ipo nafasi ya 14 pointi 41 inavutwa shati na Lipuli ipo nafasi ya 17,Mwadui ipo nafasi ya 15, Alliance nafasi ya 16 zote pointi 41./ Yanga inapambania nafasi ya pili ikiwa nafasi ya pili na pointi 68 inavutwa shati na Azam FC yenye pointi 66 ikiwa nafasi ya tatu.

Safu ya ushambuliaji ya Mtibwa Sugar imefunga mabao 27/ Yanga mabao 43. Pande wa safu ya ulinzi Mtibwa imefungwa mabao 32/Yanga 27

KMC v Tanzania Prisons, Complex/ zote mbili hazina uhakika wa kubaki ndani ya ligi, KMC ipo nafasi ya 11 pointi 46/ Prisons ipo nafasi ya 12 ina pointi 45 ambazo zinaweza kufikiwa na Mbao FC

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic