April 5, 2019






NA SALEH ALLY
TANGU timu ya taifa, Taifa Stars ifanikiwe kushinda nafasi ya kucheza katika Kombe la Mataifa Afrika (Afcon), kwa mara ya pili, kumekuwa na muunganiko mkubwa wa Watanzania kupitia kila nyanja na muunganiko mkuu ukabaki kwenye michezo na hasa soka.

Kama unakumbuka, wasanii wa muziki, uigizaji nao walishiriki katika hamasa na ndio maana unaona muunganiko wa wapenda michezo na soka, wale wa burudani ukafanya Uwanja wa Taifa ushindwe kuhimiliki vishindo baada ya watu kukosa nafasi siku mechi ikipigwa.

Muunganiko huu, umefanya mchezo wa soka uendelee kuwa gumzo wakati Tanzania ikielekeza tena macho yake katika mechi ya Ligi ya Mabingwa Afrika hatua ya robo fainali wakati Simba inakwenda kuivaa TP Mazembe kesho Jumamosi.


Gumzo la mechi hiyo nalo limekuwa kubwa, kila upande ukionyesha nia ya kufanya vema, lakini muigizaji Steven Mengere anaonekana kuchafua hali ya hewa.


Siku chache zilizopita Mengere maarufu kama Steve Nyerere alikuwa akihojiwa na kituo kimoja cha runinga ya mtandaoni. Alizungumza mambo kadhaa kuhusiana na soka lakini kuhusu Msemaji wa Klabu ya Simba, Haji Manara.


Steve Nyerere hakuishia hapo, alisonga zaidi hadi kwa mashabiki wa Simba ambao hakika aliwakosea heshima, jambo ambalo hatupaswi kuacha lipite hivi maana litakuwa funzo linalotuzuia kukosea kwa mara nyingine.


Alieleza jambo zuri, kwamba atawaunga mkono Simba dhidi ya TP Mazembe na watashirikiana kuhakikisha wanashinda licha ya kwamba yeye si Simba. Hili ni jambo zuri kwa kuwa zaidi anaonyesha ni mzalendo.


Maneno haya ya Steve Nyerere yanaweza kubaki kuwa mfano mzuri hata hapo baadaye na kuonyesha kwamba alikuwa tayari kuishangilia Simba wakati yeye si Simba lakini ni kwa sababu ya uzalendo, hivyo wasio wazalendo wabadilike.


Baada ya hapo, Steve Nyerere aliulizwa kuhusiana na Manara, alichokisema kuhusiana na Manara kuwa ni mtu wa hovyo kwangu naona si kitu kibaya kwa kuwa zaidi ni utani wao ambao naujua unaendelea mara kwa mara kwa kuwa ni maswahiba.

Alichokosea ni pale alipotumbukia katika suala la mashabiki akiwazungumzia wale wa Yanga na Simba. Baadaye akasema anajua Watanzania idadi yao ni milioni 57 (hatujui alikoitoa). Akasema mashabiki wa Yanga wako milioni 39, lakini Simba wako milioni 3.4 na kati ya hao mashabiki wa Simba, mashabiki milioni 2.1 ni Waarabu.


Hii maana yake nini, Waarabu si Watanzania, hawapaswi kuwa mashabiki? Timu yenye mashabiki wa aina hiyo si ya Tanzania? Hakika ni jambo baya sana kuzungumzwa na mtu anayejitambua na hasa kwa mtu kama yeye Steve Nyerere ambaye anaonekana ni kama kiongozi na ameshiriki kwenye uongozi hadi wa Bongo Movie.


Maana yake, Waarabu si watu? Hawana haki ya kushangilia mpira? Wakiwa katika timu wanapaswa kugawanywa kwa idadi yao? Kinachosikitisha zaidi, maneno ya kibaguzi anayoyatoa, yalipigwa vita sana mwanzoni na Mwalimu Julius Nyerere ambaye yeye sasa anatumia jina lake bila ya kibali.


Huenda hili watu wengi wameliona ni kama jambo la kawaida sana, lakini Steve Nyerere anapaswa kuamka na wengine muangalie ujinga huu usije ukarudia wakati mwingine, ni jambo baya sana kurejesha ubaguzi na tena michezoni.


Michezo inaunganisha watu, inawafanya wengi wajisikie kuwa pamoja. Hivyo si sahihi kuanza kuzungumza maneno makali na mabaya kwa kigezo cha utani, yaani alikuwa akimtania Manara. Vema kuangalia wakati wa utani ni wapi au kipindi gani.


Kiungwana Steve Nyerere kama anaamini uungwana ni vitendo na uanadamu bora basi anapaswa kuwaomba radhi wale ambao anaamini ni Waarabu aliokuwa akiwataja.

Pia nimsisitize licha ya kwamba ni rafiki yangu na tunaheshimiana, lazima awe makini na maneno anayozungumza maana mbeleni anaweza kukwama katika ndoto anazotaka kuzitimiza kwa watu kumkumbusha maneno au matendo ya kijinga aliyoyafanya kabla.


13 COMMENTS:

  1. Usimlazimishe mtu kuipenda Simba.... Ila yeye ni mtazamo wake hayo mengine unaongezea wewe.... Wewe mbona huwa unatuongopea humu.....wewe ni mshabiki wa simba.... Usitulazimishe

    ReplyDelete
  2. Usimlazimishe mtu kuipenda Simba.... Ila yeye ni mtazamo wake hayo mengine unaongezea wewe.... Wewe mbona huwa unatuongopea humu.....wewe ni mshabiki wa simba.... Usitulazimishe

    ReplyDelete
  3. Unaona ujinga wa nyerere tu huo ujinga wa manara kuwasema wakongo nisawa acha moyo uende upendapo

    ReplyDelete
  4. Changia point, Alilosema hata mimi sijalipenda ni ubaguzi ambao si mzuri, unajenga chuki na ubaguzi ndan yake. Msanii ni kioo cha jamii unapooongea kitu jiulize mara mbili na uangalie na athari zake

    ReplyDelete
  5. Sareh wewe ni mmbea sana mbona hakuna issue hapo. Steve yuko sahihi ila ww ndo unakuza mambo.

    ReplyDelete
    Replies
    1. Aombe radhi,tukiendekeza mihemukobya kishabiki bila kujua shabaha ya uzalendo wetu, leo uarabu tunaukalia kimya,kesho tutaingiza uchaga,uzinza,ujita,uhehe.aombe radhi.

      Delete
  6. Ujinga wa Manara huoni eeee,,,,umeumia kwa Hilo wee poleni Sana ila ndo ukweli huo nyie mijitu mweusi mnajipendekeza Tu kushabikia simba

    ReplyDelete
  7. Saleh hakika wew c mwandishi bali mnazi tuu ,next time tumia cerebrum vizuri

    ReplyDelete
  8. Mashsbiki wote wa Manchester United ni Wazungu? Mashsbiki wote wa Liverpool ni wazungu? Mashabiki wa Buyern Munich ni wajerumani au wazungu? Mashsbiki wote wa Barcelona ni waspania? Mashsbiki wote wa real Madrid ni waspania? Pengine wewe mtanzania povu linakutoka kwa Manchester United yako hata huko uengereza unakusikia jina tu vipi leo unakwenda kumzodoa mtanzania kwa maneno ya kipumbavu na Simba yake ya Tanzania? Salehe Jembe yupo sahihi kabisa kulileta hili jambo na tunapaswa kulikemea kwa nguvu zetu zote. Huwezi kuzungumza au kuunga mkono ujinga wa maneno ya kibaguzi ya kipumbavu kama aliyoyazugumza Steve Nyerere juu ya mashabiki wa Simba kama wewe mwenyewe si mpumbavu na msenge wa akili. Kufulia kwa Yanga isiwe nongwa ya kuitakia mabaya Simba vile vile. Mashsbiki wa Simba na Simba yao watabakia kuwa Juu Tanzania na roho mbaya kamwe haijengi kitu na ndio maana migogoro haindoki upande wa pili. Hasada sio kitu kizuri hata kidogo watanzania tuachanane na maneno ya chokochoko ya kibaguzi.

    ReplyDelete
  9. Du hivi kumbe yanga hayurusu watu wenye asili ya nje but watanzania hakuna kushabukia hii timu,huyu mnaye mlilia kila siku ni black kanjibay

    ReplyDelete
  10. KWANI TATIZO NINI ? WAARABU? AU WAHINDI? ACHENI UBAGUZI USIO NA MAANA. YANGA KUNA BIN KLEB, KUNA YULE MKUU WA SPOTI PESA WALE NA HAO WA SIMBA TOFAUTI ZAO NINI? MANJI MZARAMO? ACHENI UPUUZI WA KUBAGUANA KWA RANGI, MATAIFA,MAKABILA AU UDINI. HUYU JAMAA AAMBIWE THATS TOO LOW.

    ReplyDelete
  11. Anaeona steve yupo sawa atakua ana matatizo. Hiyu jamaa huwa simwelewi ni nani kwenye taifa maana kama uigizaji hajui anachojua michango ya misiba tu huyu hana lolote

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic