July 29, 2019



BENO Kakolanya, mlinda mlango wa Simba ameanzishiwa program maalumu itakayomfanya awe fiti msimu ujao akiwa nchini Afrika Kusini.

Kakolanya amesajiliwa na Simba msimu huu akitokea Yanga kwa kandarasi ya miaka miwili ana kazi ya kumuonyesha Kocha Patrick Aussems msimu ujao ili kupenya kikosi cha kwanza kwa kumuweka benchi Aish Manula.

Kakolanya amesema kuwa ana furaha kuwa ndani ya kikosi cha Simba ana imani kubwa ya kufanya vema msimu ujao.

“Huku tunapambana kujiweka sawa na kila mchezaji anaendelea vizuri kwa kuwa sawa kwa ajili ya msimu ujao na imani ni kubwa kwamba tutapambana.

“Suala la namba kwa sasa sio kipaumbele changu kwa kuwa mimi sipangi kikosi hilo lipo mikononi mwa mwalimu cha msingi ni mashabiki kuzidi kutuombea,” amesema Kakolanya.


1 COMMENTS:

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic