July 16, 2019



UONGOZI wa KMC ambayo ilikuwa inashiriki michuano ya Kagame nchini Rwanda umesema kuwa kwa sasa nguvu zote ni kwenye maandalizi ya Ligi Kuu Bara inayotarajiwa kuanza Agosti 23.

KMC kwenye michuano ya Kagame imekusanya pointi tatu baada ya kucheza michezo mitatu ambapo ilipoteza mbele ya TP Mazembe kwa kufungwa bao 1-0 ilishinda mbele ya Rayon Sports kwa bao 1-0 na kulazimisha sare ya kufungana bao 1-1 dhidi ya Atlabara kwenye kundi A.

Akizungumza na Saleh Jembe, Ofisa Habari wa KMC, Anwar Binde amesema kuwa ushindani ulikuwa mkubwa na wanaamini kuna kitu wamejifunza.

“Timu ilikuwa inajenga muunganiko mpya hivyo wachezaji wamepambana kwa uwezo wao na nimependa namna ambavyo wamefanya kitu kizuri.

"Kwa sasa timu itaweka kambi Dar na kama itatokea itakuwa nje ya hapo tutatoa taarifa mapema kikubwa sapoti na maandalizi ya ligi kwa msimu ujao," amesema.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic