October 14, 2019



UONGOZI wa Azam FC umesema kuwa kichapo cha mabao 5-0 walichoshusha mbele ya GreenWarriors ni manyunyu tu kuelekea kwenye mchezo wao wa ushindani dhidi ya Simba utakaochezwa Octoba 23 uwanja wa Uhuru.

Azam FC iliwatumia wachezaji wake wengi ambao hawajapata nafasi kwa muda ikiwa ni pamoja na nahodha Agrey Moriss aliyekuwa majeruhi, Seleman Ndikumana na Kassim Khamis ambao walikuwa hawapati nafasi kikosi cha kwanza.

Akizungumza na Saleh Jembe, Idd Cheche, kocha msaidizi wa Azam FC amesema kuwa ni hesabu za timu kuzidi kutengama hasa wakati ambao ligi imesimama jambo litakaloimarisha kikosi kuwa cha ushindani.

“Huu ni mwanzo tu kwani kwa sasa ligi imesimama na tuna jiaandaa na mchezo wetu dhidi ya Simba, bado kikosi kinaimarika na tunaamini tutakuwa imara kwenye michezo yetu yote ya ligi huu ni mwanzo tu,” amesema Cheche.

Mabao ya Azam mbele ya GreenWarriors uwanja wa Azam Complex yalifungwa na Abdlkassim Khamis alitupia mawili huku Donald Ngoma,Richard Djod na Seleman Ndikumana wakitupia mojamoja na leo watakuwa uwanja wa Uhuru kuivaa African Lyon.

2 COMMENTS:

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic