October 13, 2019



MOHAMED Hussein, Mmachinga, mshambuliaji wa zamani wa timu ya Yanga na timu ya Taifa amesema kuwa kikwazo kikubwa kwa mshambuliaji wa Yanga, David Molinga ni ubonge wake tu ila kiuwezo yupo vizuri.

Molinga ndani ya dakika ya 270 ambazo ni sawa na mechi tatu ametupia jumla ya mabao mawili, ambapo moja alipachika kwa kichwa na lingine kwa mpira uliokufa kwenye mchezo mmoja dhidi ya Polisi Tanzania Uwanja wa Uhuru.

Akizungumza na Saleh Jembe, Mmachinga amesema kuwa amemfuatilia kwa ukaribu Molinga na kugundua kuwa ubonge wake unampa uzito wa kufanya maamuzi akiwa ndani ya uwanja.

“Molinga ana sifa za ushambuliaji hasa pale anapoamua kucheza namba tisa analijua lango na ana uchu wa kufunga ila tatizo lake lipo kwenye uzito anashindwa kuwa na maamuzi ya haraka kwake kila kitu ni kizito.

“Anajipa majukumu mengi akiwa uwanjani kiasi kwamba unashindwa kujua anacheza namba ngapi muda mwingine unamkuta yupo kwenye namba 10 wakati mwingine nyuma sasa hapo kama ataendelea itampa wakati mgumu kufikia malengo, lakini akitulia na asipopata majeruhi atafunga mabao mengi,” amesema Mmachinga.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic