November 15, 2019



UONGOZI wa Kagera Sugar umesema kuwa kwa sasa ni lazima wapambane kuendelea na moto wao ambao wameanza nao msimu huu kwa kupata matokeo chanya kwenye mechi zao zote watakazocheza.

Mecky Maxime, Kocha Mkuu wa Kagera Sugar amesema kuwa wanatambua ushindani uliopo ndani ya ligi jambo linalowafanya wapambane kuendeleza wimbi la ushindi kwa timu.

“Ligi ni ngumu na kila timu inahitaji matokeo jambo ambalo linafanya nasi tupambane kupata ushindi kwani hakuna mwalimu ambaye anaipeleka timu uwanjani akifikiria kupoteza mchezo wake.

“Kikubwa kilicho nyuma ya mafanikio ni wachezaji kujitambua na kutimiza majukumu yao kwa wakati kwani kila mchezaji ana kazi yake ndani ya uwanja ni suala la muda tu kupata matokeo chanya," amesema.

Kagera Sugar ipo nafasi ya pili ina pointi 22 ikiwa imecheza jumla ya mechi 10 ikipoteza mechi mbili na kutoa sare mbili na imeshinda jumla ya mechi sita.



0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic