November 12, 2019



PEP Guardiola, Kocha Mkuu wa timu ya Manchester City amewashushia lawama waamuzi wote wa mchezo wao wa Ligi Kuu England mbele ya Liverpool uliochezwa Anfield kwa kusema kuwa umeegemea upande mmoja wa timu.
Mabingwa hao watetezi wa Ligi Kuu England walishindwa kuivunja rekodi ya Liverpool kucheza bila kufungwa kwa muda wa siku 900 wakiwa Anfield na kwa kupokea kichapo cha mabao 3-1 huku Guardiola akidai walistahili kupewa penalti mbili.
Mwamuzi wa kati Michael Oliver ndiye ambaye alikuwa na jukumu la kuamua wapewe penalti au la alipeta na kuwaruhusu kucheza jambo lililomfanya Guardiola raia wa Hispania  avimbe kwa hasira na kumuonyesha ishara ya vidole viwili mwamuzi wanne Mike Dean kumueleza hali halisi akidai Alexander Anorld aligusa mpira.
Meneja wa Liverpool, Jurgen Klop amesema kuwa hakuona kama kulikuwa na mazingira ya penalti ila alishtushwa na goli la kwanza la mchezaji wake Fabinho kabla ya Mohamed Salah kufunga bao la pili ambalo hajawahi kuliona kwa wachezaji wake ambao walipambana kupata bao  la tatu kupitia kwa Sadio Mane.
City ilipata bao kupitia kwa Bernardo Silva, ushindi huo unaifanya Liverpool kufikisha jumla ya pointi 34 ikiwa nafasi ya kwanza huku City ikiachwa kwa jumla ya pointi 9 ikiwa na pointi 25 nafasi ya nne baada ya kucheza mechi 12.
                                                          


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic