NIMEFURAHI
kuona Kocha Mkuu wa timu ya Taifa ya Tanzania ni Etienne Ndayiragije ambaye
awali alikuwa ni Kaimu Kocha Mkuu kwa
kupokea kijiti cha Emmanuel Ammunike ambaye alisitishiwa mkataba wake.
Kumpa
kandarasi ya kudumu ni kitu cha msingi ambacho kinastahili pongezi hasa kwa
wakati huu ambao taifa linatafuta mafanikio kwenye mchezo wa soka ambao ni namba moja kwa
kupendwa na mashabiki.
Mtihani wake
wa kujigawa pande mbili akitimiza majukumu yake ya kufundisha kwa sasa
umemalizika anabakiwa na kibarua kimoja tu kutimiza kazi kwa sasa tofauti na
awali.
Ikumbukwe
kuwa awali alikuwa ana kibarua cha kutoa madini ndani ya klabu ya Azam FC ambayo kwa wakati huo ilikuwa na
majukumu ya kitaifa na Kimataifa kwenye Kombe la Shirikisho Afrika.
Pia alikuwa
anainoa timu ya Taifa ya Tanzania jambo ambalo lilikuwa linamfanya awe bize
muda mwingi kuandaa programu mbili tofauti kwa wakati mmoja akiwa yeye ndiye
bosi.
Sasa kazi
kwake inabaki moja kwa kuwa amekabidhiwa mikoba rasmi kuinoa Stars ambayo ni
timu pendwa kwa watanzania kutokana na kuwakilisha nchi kwenye mashindano ya
Kimataifa.
Uwezo wake
ni mzuri sina mashaka nao kwani vikwazo vingi ameweza kuvivuka licha ya ubutu
wa safu ya ushambuliaji ambalo ni janga la Taifa linahitaji kutafutiwa ufumbuzi
hasa kwa wachezaji kuwa makini.
Washambuliaji
wengi wamekuwa na papara wanapofika kwenye lango jambo ambalo limekuwa
likiwafanya wakose nafasi nyingi za wazi kwenye mechi zao wanazocheza.
Ndayiragije
anawaamini vijana katika kazi na amekuwa akiwatumia kwa muda mrefu jambo ambalo
linamfanya awe karibu na wachezaji ambao wanahaha kutafuta mafanikio ya taifa.
Anawajua
wachezaji wengi ndio maana ana mchanganyiko wa wale wakongwe ambao wana uzoefu
kwa muda mrefu kwenye ligi pamoja na mashindano ya kimataifa kiujumla.
Mwelekeo
umeanza kuonekana kwani ameweza kuanza kufanya vema kwa kuipeleka timu kufuzu
michuano ya Chan nchini Cameroon 2020 sio hatua ya kubeza kwa hilo.
Tumpe sapoti
watanzania tusimtenge kwa kumuachia mzigo mzito kwani kufundisha timu peke yako
bila sapoti ya mashabiki haileti ile morali ya ushindani jambo ambalo linaumiza
kwa mwalimu na wachezaji pia.
Tushikamane
kwelikweli katika hili bila kuleta zile itikadi ambazo hazina maana kwa
mashabiki na wadau wa soka haitapendeza katika hilo inamaliza uhondo wa mpira.
Tutoe
tofauti zetu na kuziweka kando sisi wote ni ndugu na tuna kazi ya kufanya kwa
ajili ya maendeleo ya Taifa letu ambalo bado linasaka maendeleo kwa sasa
kusonga mbele zaidi ya hapa.
Kila kitu
kinawezekana kwa wachezaji wetu kupata matokeo kwani Ijumaa sio mbali ambapo
wapinzani wetu kutoka Guinea watashuka uwanja wa Taifa kuchanga karata ya
kwanza kutafuta ushindi.
Nasi pia
inatupasa tutambue kwamba tunahitaji nafasi ya kufuzu Afcon kwani ni heshima na
ni furaha kwa kila mtanzania kuona timu inapata matokeo chanya kwenye mechi za
kimataifa.
Kikubwa
kujituma kwa wachezaji wakiwa ndani ya uwanja kutasiaidia kupatikana kwa
matokeo haraka tukiwa nyumbani kwani uwanja wetu tumeshauzoea na mashabiki zetu
tunajua wanataka nini.
Wachezaji
majukumu yenu uwanjani haina haja ya kuleta ubishoo ni mwendo wa kazi mwanzo
mwisho kutafuta heshima na matokeo ndani ya uwanja kishujaa.
Kwa sasa
miguu yenu imeshikilia furaha ya mashabiki na taifa kiujumla mnapaswa mtumie
vema maelekezo ambayo mnapewa kutimiza majukumu kwa wakati.
Kile
mnachofundishwa kikae akilini na wakati mwingine mambo yakiwa magumu basi kuna
umuhimu wa kutumia mbinu ya pili kutafuta matokeo uwanjani ili kuweka heshima.
Hakuna
ambaye anafikiria kuona tena wachezaji mtakuwa na papara mkiwa langoni yale
makosa yaliyopita mnapaswa myarekebishe kwa kiwango kikubwa.
Mashabiki wanahitaji kuona timu inapata matokeo na kuwa
na morali ya kuendelea kujitokeza kwenye mechi nyingine msiwaangushe mashabiki
zetu na taifa kwa ujumla.
Benchi la
ufundi kazi kwenu kuwapa mbinu mbadala mkikumbuka kwamba mechi ya mwisho
nyumbani mlipoteza kwa kufungwa bao moja ambalo lilidumu mpaka mwisho wa
mchezo.
Wasudan
waliipoteza ile furaha ya mashabiki uwanja wa taifa kwenye mchezo wa kuwania
kufuzu Chan licha ya kwenda kupindua meza kibabe bado kulikuwa na nafasi ya
kuwatoa wapinzani wetu kwanza nyumbani kabla ya kuongeza presha mchezo wa
marudio.
Mmeshikilia
furaha ya mashabiki kwa sasa mna kazi ya kuonesha kwamba hamkubahatisha kupindua
meza kibabe nchini Sudan licha ya kuanza kwa kuchechemea mchezo wa kwanza.
0 COMMENTS:
Post a Comment