January 3, 2020



MERIH Demirah, beki wa Juventus ameingia kwenye rada za kuwindwa na Arsenal iliyo chini ya Mikel Arteta.
Bosi huyo mpya ndani ya Arsenal amesema kuwa anahitaji kuongeza nguvu kubwa kwenye safu ya ulinzi ili kuimarisha kikosi chake.
Mpaka sasa Arsenal imefungwa jumla ya mabao 30 ndani ya Ligi Kuu England jambo linalomtisha kocha huyo aliyewatungua Manchester United mabao 2-0 na ipo nafasi ya 10 kwenye msimamo.
Licha ya David Luiz na Kieran Tierney kusaini ndani ya Arsenal msimu uliopita bado hawajawa na safu imara ya ulinzi jambo linalomfanya Arteta kumfikiria Demiral mwenye miaka 21 kujibu tatizo la safu yake ya ulinzi.
Akiwa Juventus iliyo chini ya Maurizio Sarri alianza kwenye mechi nne za mwisho za kikosi hicho hivi karibuni.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic