January 3, 2020


UONGOZI wa Klabu ya Singida United umetangaza kuingia mkataba wa miezi sita na wachezaji Haruna Moshi ‘Boban’, Haji mwinyi aliyekuwa KMKM ya Zanzibar na Tumba Lui ili kukiongezea nguvu kikosi hicho kilicho mkiani mwa msimamo wa Ligi Kuu Bara msimu huu.

Singida mpaka sasa imeshakamilisha usajili wa wachezaji sita ikiwa ni katika harakati ya kukinusuru kikosi hicho kinachoonekana kuwa dhoofu msimu huu.

Ofisa Habari wa Singida United, Cales Katemana, amesema kuwa bado wanaendelea kukiimarisha kikosi chao kuendana na mapendekezo ya kocha, Ramadhan Nswanzurimo.

“Tunaendelea kufanya usajili kuendana na mapendekezo ya mwalimu na hivi tumekamilisha usajili wa Boban na wenzake ambao wamejiunga nasi kwa mkataba wa miezi sita.

“Kwa sasa tumeweka nguvu katika kusajili wachezaji wenye uzoefu kwa kuwa tunaamini kwa uzoefu walionao wataisaidia timu kufanya vizuri kwenye michezo yetu ijayo,” amesema Katemana.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic