JANUARI
mwaka huu, Mbwana Samatta aliandika historia kwa kuwa Mtanzania wa kwanza
kucheza Ligi Kuu ya Engalnd maarufu kama Premier baada ya kusajiliwa na Klabu ya
Aston Villa.
Ni dhahiri
kuwa Kocha wa Aston Villa, Dean Smith aliona mbali sana kwa kuamua kumvuta
Samatta kutoka KRC Genk ya Ubelgiji kutokana na ubora alionao mshambuliaji huyo
raia wa Tanzania.
Ujio wa
Samatta ndani ya Aston Villa unaweza kuwa na faida au hasara kwa timu hiyo
wakati huu ikiwa katika harakati za kujiokoa na janga la kushuka daraja.
Kwa sasa
Premier imesimama kutokana na tahadhari ya maambukizi ya Virusi vya Corona
ambavyo vimesababisha mikusanyiko yote inayohusisha watu wengi kupigwa marufuku
ikiwemo michezo.
Mpaka Premier
inasimamishwa kwenye, Aston Villa ipo nafasi ya 19 ikiwa imekusanya alama 25 tu
katika mechi 28.
Kutokana na
Aston Villa kuyumba na kuwa mguu ndani mguu nje kwenye Premier, kuna baadhi ya
timu zinaonekana kummezea mate Samatta huku ikitajwa kuwa huenda staa huyo
mwisho wa msimu huu akaondoka kikosini hapo.
Kuna timu
zimetajwa kwamba huenda ndipo Samatta akatua huko. Timu zenyewe hizi hapa;
Tottenham
Kwa miaka
mingi, Tottenham maarufu Spurs imekuwa ikimtegemea zaidi Harry Kane katika
ufungaji, hili limeonekana kuwagharimu sana msimu huu baada ya staa huyo kuwa
majeruhi kwa kipindi kirefu.
Kane ndiyo
namba tisa pekee ambaye walikuwa wakimtegemea na baada ya kuumia ikabidi Kocha Jose
Mourinho kuamua kumtumia Heung-min Son ambaye naye akapata majeraha.
Lucas Moura
sio straika, lakini yupo Troy Parrott ambaye naye anaonekana bado hayupo sawa,
hivyo hapa unaiona nafasi ya Samatta iko wazi kabisa kwenda kuwa mbadala sahihi
wa Kane.
Crystal Palace
Akiwa Genk,
iliwahi kutajwa kuwa Crystal Palace inamuwinda Samatta. Msimu huu Crystal
Palace msimu huu wameonekana kuwa na mastraika ambao hawana muendelezo mzuri.
Mfano mzuri
ni Christian Benteke ambaye amekuwa hana jipya kutokana na kugubikwa na ukame
wa mabao tangu msimu uliopita, Jordan Ayew licha ya kufunga mabao nane, lakini
ni straika ambaye pia hana muendelezo mzuri katika kufunga.
Ukija kwa
upande wa Wilfred Zaha yeye ni winga na licha ya kupambana hatakiwi kutegemewa
peke yake katika kufunga kwa sababu si mshambuliaji halisi.
Kocha Roy
Hodgson anapambana kuhakikisha anaondokana na tatizo la ukame wa mabao kwenye
kikosi chake na ndio maana alimchukua kwa mkopo, Mturuki, Cenk Tosun kutoka
Everton, lakini bado hajapata anachotaka.
Kama Tosun
hatapata nafasi ya kusajiliwa moja kwa moja basi, Samatta anaweza kuwa
suluhisho la ufungaji ndani ya timu hiyo.
Chelsea
Tayari Kocha
Frank Lampard ana Tammy Abraham, Michy Batshuayi na Oliver Giroud katika kikosi
chake cha Chelsea, ukiona hivyo unaweza kudhani kocha hana wazo la kusajili straika
mwingine.
Kwa msimu
huu, Abraham tu ambaye anaonekana yuko juu kwa kufunga mabao, Batshuayi alianza
vizuri, lakini bado anaonekana kutomshawishi Lampard, Giroud alionekana kuwa
wamoto kabla ya ligi kusimama. Mkataba wake unamalizika mwishoni mwa msimu huu.
Licha ya
Abraham kufunga mabao 13 mpaka sasa, lakini Lampard atahitaji kuongeza nguvu
kwa kuleta straika mwingine na jicho lake linaweza kumuangalia Samatta licha ya
sasa kuripotiwa kuwa wanamfuatilia Moussa Dembele wa Lyon.
Everton
Dominic Calvert-Lewin
amefunga mabao 13 kwenye Premier msimu huu, kwa mfumo anaoutumia Kocha wa
Everton, Carlo Ancelotti ambao ni 4-4-2, mshambuliaji huyo kwa sasa
anachezeshwa na Richarlison wakati huu ambapo Oumar Niasse akishindwa kuonyesha
cheche zake.
Kama Villa
itashuka daraja, basi Everton watakuwa na nafasi ya kumsajili Samatta na endapo
atachezeshwa na Calvert-Lewin na Richarlison itakuwa bonge la kombinesheni kwa
kocha Ancelotti.
Arsenal
Wengi
wanaweza kushangaa inawezekanaje wakati huu Samatta kukipiga Arsenal, lakini
sikiliza hii; Pierre-Emerick Aubameyang mkataba wake unamalizika msimu ujao na
kuna uwezekano akaondoka, Alexander Lacazette msimu huu kiwango chake bado sio
cha kuridhisha.
Gabriel
Martinelli na Eddie Nketiah bado ni makinda ambao Kocha Mikel Arteta anawaandaa,
hivyo kama wakifanya chaguo la kumsajili Samatta itakuwa sahihi kutokana na
ufinyu wa bajeti yao.
Unajifariji tu...wala hakuna timu ya kumnunua yy ateremke daraja tu
ReplyDeleteAnataka kutufanya wajinga wakati hakuna hata timu moja iliyoonyesha nia
ReplyDeleteDu wabongo kwa kuwa madalali hatujambo. Sa samatta amefanya nini kimya hapo hadi aende spurs, asenal na chelsea. Acheni kupromo vitu vya uongo
ReplyDelete