May 8, 2020

BIASHARA United ya mkoani Mara ipo nafasi ya 10 ikiwa na pointi 40 kwenye Ligi Kuu Bara.

Safu yake ya ushambuliaji imefunga mabao 21 huku safu yake ya ulinzi ikiwa imeruhusu mabao 22 baada ya kucheza mechi 29.


Mwenyekiti wa Biashara United, Seleman Mataso amesema kuwa kwa sasa wakati wa mapumziko ya lazima yaliyosababishwa na Virusi vya Corona vijana bado wanaendelea kufanya mazoezi binafsi wakiwa nyumbani.

"Vijana wanaendelea kufanya mazoezi binafsi wakiwa nyumbani kwa sasa lengo ni kuona kwamba ligi ikirejea nao wanakuwa kwenye ubora wao," amesema.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic