SERGIO Ramos, nyota wa Klabu ya Real Madrid inaele
zwa kuwa timu yake haina mpango wa kumpa ofa ya mkataba mpya nyota huyo.
Ramos mwenye miaka 34 mkataba wake unameguka mwishoni mwa msimu huu na inaelezwa kuwa anaweza kuibukia kukipiga nchini China.
Alijiunga na Real Madrid akitokea Klabu ya Sevilla amebakiza mabao tisa pekee ili kufikisha mabao 100 kwani kwa sasa amefunga jumla ya mabao 91 ndani ya Madrid.
Licha ya kuwa Kwenye ubora wake msimu huu akiwa na klabu hiyo kwa kucheza mechi 34 na kutupia mabao saba bado halijawashtua mabosi wa Real Madrid.








Sijaelewa, Ramos ni mshambuliaji?
ReplyDeleteHata Mimi nimeshangaa!!!
Deletehii habari ni kweli? beki tena wa kati ana mabao 91 duuu hatari
ReplyDelete