June 28, 2020

HISTORIA inasema kuwa Liverpool mara ya mwisho kuwa Mabingwa wa Ligi Kuu England ilikuwa ni mwaka 1989/90 baada ya kuchukua sasa wanakuwa na mataji 19 kibindoni. 

Msimu wa 2019/20 imeandika historia ya kutwaa taji la Ligi Kuu England baada ya miaka 30 likiwa ni taji la Kwanza tangu Ligi hiyo ianze kuitwa Premier mwaka 1992.

Kocha Mkuu, Jurgen Klopp ameweza kuweka rekodi matata kwa msimu wa 2019/20 ambapo ameonekana kuwa bora baada ya kujikusanyia pointi 86.

Ameshinda jumla ya mechi 28 amelazimisha sare mechi mbili huku akipoteza mechi moja kati ya 31 ambazo amecheza.

Inatwaa ubingwa mapema ikiwa na mechi saba mkononi ila watashindwa kusherehekea  ubingwa kutokana na janga la Virusi vya Corona.

Klopp amesema:"Sijasubiri kwa miaka 30, nimekuwa hapa kwa miaka minne, lakini nimefanikiwa hasa katika miezi hii mitatu ambayo tulipumzika, hakuna ambaye alijua kama itatokea."

1 COMMENTS:

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic