June 30, 2020



HARUNA Niyonzima, kiungo mshambuliaji wa Yanga amesema kuwa wana imani ya kuibuka na ushindi mbele ya Kagera Sugar kwenye mchezo wa Ligi Kuu Bara utakaochezwa, leo, Julai 30, Uwanja wa Taifa.

Mchezo huo unatarajiwa kuwa na ushindani mkubwa kwa kuwa Yanga ilipoteza mchezo wa kwanza wa Kocha Mkuu, Luc Eymael kwa kuchapwa mabao 3-0 na Kagera Sugar, Januari 15, Uwanja wa Uhuru kwenye mchezo wa Ligi Kuu Bara.

Akizungumza na Spoti Xtra, Niyonzima ambaye alifunga bao lililoipa nafasi Yanga kushiriki hatua ya robo fainali mbele ya Gwambina FC, alisema kuwa wapo tayari kwa ushindani.

“Ukizungumzia mchezo wa ligi ambao tulipotezwa ni tofauti na tutakavyokutana na Kagera Sugar kwenye Kombe la Shirikisho, huku kwenye ligi tuna hesabu zetu tunakamilisha ila huku kwenye FA lazima tupambane ili tuchukue kombe.

“Walitufunga hatukatai ila wasitarajie wataweza kutufunga tena tutakapokutana, makosa ambayo tuliyafanya tumeyafanyia kazi na tutapambana,” alisema Niyonzima.

Mshindi wa mchezo wa Yanga na Kagera Sugar atakutana na mshindi wa mchezo kati ya Simba na Azam FC hatua ya nusu fainali.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic