September 2, 2020

 


UONGOZI wa simba umesema kuwa taarifa zinazoenea mitandaoni na kwenye baadhi ya vyombo vya habari zikieleza kuwa mchezaji wao nyota Meddie Kagere amepigana na Kocha Mkuu Sven Vandenbroeck sio za kweli.

Akizungumza na Saleh Jembe, Ofisa Habari wa Simba Haji Manara amesema kuwa kumekuwa na taarifa ambazo zinasambaa kwenye mitandao ya kijamii zikieleza kuwa Kagere na Sven wamepigana jambo ambalo ni la kupikwa.

"Kwetu sisi Simba ni furaha siku zote na mambo hayo yalikuwa kitambo sio sasa kila kitu kinakwenda sawa hakuna ukweli wowote kuhusu Kagere kupigana na Sven. 

"Huo ni uogo na umepikwa kusudi na kwa nia ovu ya kutuvuruga kwa kuwa mambo ndani ya Simba ni shwari hivyo tumeshajua na hatupo tayari kuvurugwa.

"Ili kujua kwamba taarifa hizo ni za uongo zinaelza kwamba Kagere alipigana na kocha mazoezini, jana Simba hawajafanya mazoezi na wachezaji walilala baada ya kocha kusema kuwa wachezaji wamechoka kwa kuwa walisafiri kutoka Arusha mpaka Mbeya, hivyo kama wamepigana mazoezini ni uwanja gani walifanya mazoezi?.


"Muda huu ndio wachezaji wanajiaandaa kwenda kuanza kufanya mazoezi, hatukubali na hatupo tayari kuvurugwa," amesema. 

Simba ipo Mbeya ambapo iliwasili jana Septemba Mosi kwa ajili ya maandalizi ya mchezo wa Ligi Kuu Bara utakaopigwa Septemba 6, Uwanja wa Sokoine dhidi ya Ihefu FC.

23 COMMENTS:

  1. Mruhusini avae Power Bank yake.

    ReplyDelete
    Replies
    1. Uchawi simba , kubebwa na marefa simba, Simba ni TFF, simba wana wachezaji wazee, simba wanafanya mipango nje ya uwanja hivi ukijumlisha hivi vitu vyote hii si ni Taarabu jamani, aaaah aaah Taarabu fc tushawazoea, kauli mbiu ya mwaka huu tutawakeraaaaaaa

      Delete
    2. Yanga sajili na mbembwe zote za mapokezi ya wachezaji wao wanaowaita wa viwango lakini pigo la Morrison bado linawachonota kiasi kuwa na hasira mbaya za kujitia aibu.Na hakuna zaidi wanaweza kufanya zidi ya simba isipokuwa uzushi na chokochoko zidi ya simba. Hata yale mapokezi ya wachezaji wao sio kwamba wale wachezaji ni wakali kiasi hicho kwani hakuna fowadi mpya wa yanga aliekuja mwenye uwezo wa kumzidi kagere au Kris Mugalu au Charles Ilanfiya. Na hakuna kiungo wa yanga mpya aliekuja mwenye uwezo wa kuzidi chama, Louis Miqson,Larry Bwalya,miraji Athumani,Mkude,Mudhamiri yasin,Fraga. Na hakuna Beki walioileta yanga kuzidi uwezo wa unyango au wawa na Kennedy juma.Huo ndio ukweli nuna ingia kichefuchefu chana jezi ya simba,zusha kagere mchawi au mzee na kapigana na kocha wake ila simba kwa sasa itabakia kuwa simba kwenye soka la Tanzania na east Africa na utopolo wajipike kisaikolojia kuelekea ligi kuu kwani naona wana matarajio makubwa kuliko uwezo wa timu yao watakuja kulia .

      Delete
    3. Je Sven na Kagere walipigana ama hawakupigana hii ndio hoja iliyoko mezani hizo nyingine pamoja na povu jingi havina mashiko ndugu.

      Delete
  2. Kama manara anasema mambo hayo yalikuwa kitambo maana yake ilishatokea

    ReplyDelete
    Replies
    1. Kw hiyo kama yalishatokea we unatakaje, mpira hauchezwi kwenye mitandao ya kijamii kinachoonekana sasa hv utopolo wanatafuta Kick za kwenye mitandao ya kijamii kuliko kucheza mipra uwanjani. Tutawakeraaaaaaaa zaidi msimu huu

      Delete
  3. mpaka zaizi bado yanatokea isipokuwa kiukweli simba mambo yao hayavuji ovyo ila hayo mambo yapo mpaka yanasambaa mtandaoni yametoka wapi lisemwalo lipo kama halipo laja

    ReplyDelete
  4. Utopolo mmedoda uwanjani mshafeli mnatafuta ushindi nje ya uwanja hamwezi.

    ReplyDelete
  5. Enter your comment...uzush tu huo

    ReplyDelete
  6. Mpeni hirizi yake mambo yarudi kama kawaida

    ReplyDelete
    Replies
    1. Hirizi anayo si ndo mana amekuwa mfungaji bora, sasa mnataka tumrudishie hirizi gani? na mwaka huu tumemuongezea hirizi nyingine kazi mnayo siyo 4G ni 5G, tutaendelea kuwakera wenye stress zenu huku mkijifanya mna furaha shenziiiiiiiiiiiiii. This is Simba

      Delete
  7. Wamekosa cha kuongea Simba nidhamu ni kipaumbele. Walimshindwa Morisson hivyo wanadhani wote wajinga kama wao.Morisson ametulia tuli..Simba jana hawakufanya mazoezi na inadaiwa eti walipigana mazoezini jana Utopolo mpira umewashinda wamebakia na uzushi.

    ReplyDelete
  8. Anzisheni gazeti la umbeya Utopolo. Mmekuwa mabingwa wa udaku.Shigongo must be proud kupata mshindani wa udaku.

    ReplyDelete
  9. Gongowazi wanaumizwa na shuari na nidhamu ya juu iliyopo kwa timu ya Manara na wanaiombea duwa Simba nayo iwe kama hali ya mvurugano na kuzomeana kama ile waliyokuwa nayo wao. Wamechelewa

    ReplyDelete
  10. Piganeni tu kwani siyo Latina ukubali

    ReplyDelete
  11. Wazee wameshaanza kugombana huko

    ReplyDelete
    Replies
    1. USISEME WAZEEE, SEMA WAZEE WA 4G

      Delete
    2. Unawaita wazee wakati wanakupiga 4G..bado mnawashwa mtakunwa tena nyie vijana wa chips mayai

      Delete
  12. Naye alivyozungumza kuwa kuna mchezaji mmoja amekataa kulala na mwenziwe anao ushahidi?

    ReplyDelete
  13. Umeiona picha kwenye blogu hii. UJAHILI NI UGONJWA. NA UGONJWA HUU UNAITWA UTOPOLO.

    ReplyDelete
  14. Yanga ni wapuuzi sasa, wajitafakari. Mpira umewashinda imebaki kelele tuu

    ReplyDelete
  15. Gongowazi ni shida. Wameunda kundi lao la waandishi na watangazaji wa michezo kwa ajili ya kuwazushia mambo mabingwa wa nchi. Unajua kila wanachofanyanya akina Maulid Kitenge, Ricardo Momo, Yusuf Mkule na wapuuzi wengine. Leo Haji Manara amewakomesha mkabaki mnajing'atang'ata tu.

    ReplyDelete
  16. Piganeni sana manara atapinana na onyango

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic