September 3, 2020

 


BERNARD Morrison, winga mpya wa Klabu ya Simba rasmi atakipiga kwenye klabu hiyo baada ya Shirikisho la Soka Tanzania kumtambulisha kwamba ni mchezaji wa timu hiyo.

Agosti 30 kwenye kilele cha Wiki ya Mwananchi Yanga ilimtambuisha Morrison kuwa mmoja kati ya wachezaji wake 28 kwa kueleza kuwa mchezaji huyo kesi yake ipo Mahakama ya Kimataifa ya Usuluhishi wa Masuala ya Wachezaji,(Cas).

Mchezaji huyo pia Agosti 22 kilele cha Simba Day alitambulishwa kuwa mchezaji wa Simba na Agosti 30 jambo lililomfanya awe mchezaji pekee aliyetambulisha mara mbili ndani ya Uwanja Mkapa.

 

Morrison aliyekuwa na mvutano na mabosi wake hao wa zamani, alitajwa kwenye kilele cha Wiki ya Mwananchi kama mchezaji wa Yanga, akiwa jijini Arusha kukinukisha kwenye mechi ya Ngao ya Jamii ya timu yake mpya ya Simba iliyoishinda Namungo kwa mabao 2-0.

 

Lakini mashabiki wakiwa bado hawaamini kama nyota huyo aliyewapa raha msimu uiliopita kwa kuwatungua Simba katika mechi ya marudiano ya Ligi Kuu Bara, atasalia kikosini mwao, katika orodha ya usajili mpya ya TFF kwa msimu ujao jina lake limetokezea Simba kuonyesha ni mali yao rasmi sasa.

 

Ofisa habari wa TFF, Cliford Ndimbo, amesema kilichomfanya Morrison awe kwenye orodha ya Simba badala ya ile ya Yanga ni kwa kuzingatia maamuzi ya Kamati  ya Sheria na Hadhi ya Wachezaji iliyomtambulisha kama mchezaji huru baada ya kusikiliza kesi iliyomhusisha Mghana huyo na Yanga.

12 COMMENTS:

  1. Hilo limepita, ligi na ianze tuu maneno mengi ya nini?

    ReplyDelete
  2. KAMA TFF NDIO WALISUKA MIPANGO YA KUMPELEKA SIMBA ULITEGEMEA WAMUIDHINISHE AICHEZEE YANGA? DHAMBI HII ITAWATAFUNA SIMBA TFF NA MORISSON. MSIMU UJAO KUNA MTIKISIKO MKUBWA UTATOKEA KWENYE SOKA LA TANZANIA, NGUZO KUBWA ITAANGUKA.

    ReplyDelete
    Replies
    1. Hata malinzi akitoka jela Huwezi tena kugombea hivyo sahau kabisa kama zile za tff kuinyanyasa simba zitarudi

      Delete
    2. Sawa malinzi alikuwa anawanyanyasa kwa kufungwa na kagera sugar

      Delete
    3. Acha uzembe wewe yanga na simba haya mambo wanafanyiana sana tu.ATA okwi mulivunja naye mkataba na yanga hivyohivyo na raisi alikuwa malinzi na akawatetea nyie simba mumezidi dhuruma.e

      Delete
  3. tunajua mwandishi ungependa Morrison aendelee kuvaa jezi ya Yanga...acha kuendelea kuweka picha za Morrison akiwa kwenye jezi za kijana

    ReplyDelete
  4. Wamesahau walivyokuwa wakishinda kwa nguvu na kupora wachezaji wa Simba chini ya TFF ya Malinzi.Sasa haki imetawala wakudeka na waliozoea kubebwa wamekuwa mabingwa wa kulalamika.

    ReplyDelete
  5. HILI SUALA LISIISHE HIVI HIVI. HAIWEZEKANI MTU AFOJI SAINI YA MCHEZAJI HALAFU ASISHTAKIWE. NATAMANI YANGA WAENDE CAS KAMA WANAVYODAI ILI WABAINIKE NA KUFUNGIWA.

    ReplyDelete
  6. Yange yange Ni laana ya kukataa kumkopesha team manji, sasa inawatafuna

    ReplyDelete
  7. Sasa tunae GSM ambaye ni bora kuliko Manji na
    Moo anaeturejeshea furaha msimu huu na ijayo

    ReplyDelete
    Replies
    1. 😆😆😆😆 GSM ashawaliza kwa Morrison mkataba hewa, mnafurahisha kwelikweli. Atawakiza sana tu na kudanganywa sana tu.

      Delete
    2. Tutawachania hayo mavijola yenu na kumpigeni sisi hakuna utani na nyie ohoo!

      Delete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic