September 29, 2020


 

DAVID Kissu kipa namba moja wa Azam FC, ameweka rekodi ya kuwa kipa pekee kwenye Ligi Kuu Bara kucheza dakika nyingi bila kuruhusu bao lolote ambapo amecheza jumla ya dakika 360 sawa na mechi nne.

 

Kissu alijiunga na Azam FC, akitokea Gor Mahia ya Kenya alipokipiga kwa mafanikio makubwa akifanikiwa kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu nchini Kenya mara mbili kwa sasa amekuwa nguzo muhimu kwenye kikosi cha Azam ambacho hakijapoteza mchezo wowote hadi sasa kwenye Ligi Kuu Bara.

 

Kisu amekusanya ‘clean sheet’ hizo kwenye mechi dhidi ya Polisi Tanzania, Coastal Union, Mbeya City na Tanzania Prisons ambapo amecheza kwa dakika 90 kwenye mechi zote.

 

Azam FC inashika nafasi ya kwanza kwenye Ligi Kuu Bara wakikusanya jumla ya pointi 12, kwenye mechi nne walizoshuka dimbani huku wakifunga jumla ya mabao matano na wakiwa hawajaruhusu bao lolote hadi sasa.

 

2 COMMENTS:

  1. Akidumu hivyo mpaka mechi kumi na saba atakua kipa bora ila ifahamike tu kwamba kipa bora huanza na mabeki bora,bado mapema ligi haijachanganya mtakuka kumtafuta kwa tochi huyu.

    ReplyDelete
  2. Sasa kaweka Record hapo jamani, mbona unapenda sana kudanganya umma? Acha unaa

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic