September 29, 2020


 UONGOZI wa Simba umesema kuwa leo Septemba 28 utaanza mazoezi kwa ajili ya kujiweka sawa kuelekea Kwenye mchezo wa Ligi Kuu Bara dhidi ya JKT Tanzania. 


Simba itakuwa ugenini Oktoba 4, Uwanja wa Jamhuri, Dodoma ambapo itamenyana na JKT Tanzania.


Ofisa Habari wa Simba, Haji Manara amesema kuwa leo wataanza na mazoezi ya Gym kisha jioni watafanya mazoezi Uwanja wa Bunju.


"Tumetoka kushinda mabao 3-0 mbele ya Gwambina FC,  program ya Kwanza ilikuwa mapumziko jana na leo asubuhi mazoezi ya Gym na jioni tutakuwa Uwanja wa  Bunju.


"Kikubwa tunahitaji kuendelea kupata matokeo kwenye mechi zetu na mchezo wetu ujao itakuwa ni dhidi ya JKT Tanzania, mashabiki waendelee kutupa sapoti," amesema. 


Simba imetoka kushinda mbele ya Gwambina Uwanja wa Mkapa inakutana na JKT Tanzania ambayo imetoka kupoteza kwa kufungwa bao 1-0 mbele ya Coastal Union Uwanja wa Mkwakwani, Tanga.

2 COMMENTS:

  1. Piga zoezi tushindw mechi zote mzunguko wa kwanza na wapili, ubingwa bila kufungwa Wala sare zaidi Ile ya bahati mbaya dhidi ya mtibwa.

    ReplyDelete
  2. Kabisa zaidi ya ile sare haitakiwi tena ni kushinda mechi zote hadi ubingwa bila kifungwa inawezekana

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic