September 29, 2020



MANCHESTER United inasemekana wana imani watamsajili Jadon Sancho kabla ya dirisha la usajili kufungwa.

Meneja wa Manchester United, Ole Gunnar Solskjaer amemwambia nyota wa Borussia Dortmund, Jadon Sancho kuwa dili lake la kujiunga na United litakamilika kwa mujibu wa ripoti ya Dagbladet.

Mpaka sasa United walishindwa kutoa fedha ya pauni milioni 108 ambayo Dortumund wanahitaji ili wamuachie kiungo Sancho mwenye uwezo mkubwa ndani ya uwanja.

Dirisha la usajili  litafungwa Oktoba 5 lakini, Solskjaer anaonekana kuwa na ujasiri wa wa kumpata Sancho ambae ndio tageti yake ya kwanza msimu huu.

Miongoni mwa dili ambalo limezungumzwa kwa muda wote na halijaonesha mafanikio ndani ya united ni la nyota huyu aliyefunga jumla ya mabao 20 msimu uliopita na kutoa pasi 20 kwenye mashindano yote. 

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic