October 15, 2020




 MSHAMBULIAJI wa zamani wa Yanga, Mrundi, Amissi Tambwe ameibuka na kusema kuwa kitendo cha uongozi wa Yanga kumsajili mshambuliaji, Saidi Ntibazonkiza wamefanya jambo sahihi.

 

Yanga Oktoba 12 ilitangaza kumsajili mchezaji huyo kwa mkataba wa mwaka mmoja na nusu akiwa huru baada ya Oktoba 11,2020 kufunga bao pekee katika mchezo wa kirafiki wa kimataifa dhidi ya Taifa Stars akiwa na timu ya Taifa ya Burundi katika mchezo uliopigwa kwenye Uwanja wa Benjamini Mkapa jijini Dar.

 

 Tambwe amesema kuwa, wapinzani wa Yanga watakuwa na kazi kubwa ya kupambana naye kwa kuwa anamjua vizuri ubora wake huku akisisitiza Yanga ilikosa mshambuliaji anayeweza kucheza namba kumi.

 

“Nimeona kwenye mitandao wanaandika lakini najua atawasaidia ila sijajua ni kocha mwenyewe ndiyo amependekeza au hiyo ni siri yao. Kuhusu mchezaji ni mzuri, anaweza kucheza kama winga wakati mwingine mshambuliaji wa kati.

 

“Najua atawasaidia kwa sababu ukiangalia wasifu wake amecheza katika ligi kubwa hivyo ana uzoefu wa kutosha, ukiona mtu anafika huko ujue anajua na kujua anajua kweli kwa sababu tulikuwa tunafanya naye mazoezi hapa Vital’O na siku nyingi tunajuana, nafikiri wapinzani wa Yanga haswa Simba watapata shida sana,” amesema Tambwe.

11 COMMENTS:

  1. Kachaguliwa tim ya taifa kwa kuonekana mazoezini tu mchezaji mzuri lkn hakuwa na tim msim mzima watanzania tujifunze kitu

    ReplyDelete
    Replies
    1. Alikuwa amefungiwa kucheza mpira kokote kwa miaka 5 sababu ya nidhamu mbovu

      Delete
  2. Nakutupia goli la kufundishwa siyo la kufumba macho

    ReplyDelete
  3. Tambwe ana uyanga na urundi huyu

    ReplyDelete
    Replies
    1. Inaonesha Tambwe ana usongo Sana na Mnyama. Maana anamsifia mno huyu BABU Said, ila muda utazungumza

      Delete
  4. Kwa hiyo anadajiliwa kuisaidia yanga au kucheza na simba tuu?

    ReplyDelete
  5. Utopolo mtaweweseka sana kwa Simba.

    ReplyDelete
  6. Emmy mtovu wa nidham, mchezaji naye mtovu wa nidham, ha!ha!haaaa, mwishowe mwalimu + mchezaji = utopolo wote watovu wa nidham

    ReplyDelete
  7. mwambieni huyo tambwe wakati vital'o wanapigwa 6 na yy huyo said alikuepo

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic