February 9, 2021

 


KOCHA mkuu wa klabu ya Simba, Didier Gomes Da Rosa amesema kuwa mchezo uliopita dhidi ya Azam umewasaidia kujua mapungufu waliyonayo na kuyafanyia kazi kabla ya kuivaa AS Vita.

Juzi Jumapili Simba ililazimishwa sare ya mabao 2-2 dhidi ya Azam katika mchezo mkali wa kiporo cha Ligi Kuu Bara uliopigwa katika dimba la Mkapa jijini Dar es Salaam.

Simba imeondoka nchini leo kuelekea DR Congo kwa ajili ya mchezo wao wa kwanza wa kundi A, hatua ya makundi, Ligi ya mabingwa Afrika utakaopigwa siku ya Ijumaa.

Akizungumza muda mfupi kabla ya kuondoka nchini Gomes amesema: “Kwenye mchezo dhidi ya Azam tuliacha eneo kubwa wazi na kuwafanya wapinzani wetu watushambulie zaidi.

“Lakini pia tulitengeneza nafasi nyingi za kufunga ambazo tulishindwa kuzitumia, hivyo kuelekea mchezo huu dhidi ya AS Vita tumerekebisha makosa hayo na nina imani kubwa makosa hayo hatutayarudia,"


5 COMMENTS:

  1. Sio wametukumbusha, sema wametuonyesha. Wamewakumbusha kwani waliyasahau? Tumie kiswahili fasaha

    ReplyDelete
    Replies
    1. Kwan we ndo kocha... Kocha ndo anajua Kama wamesahau ama la. Umetoka ku puu hko unavamia tu unataka kujifanya we ndo unajua Sana.

      Delete
  2. tatizo kocha hakufanya maamuz sahihi kweny sub. mwenzak kaimarisha kiungo yy akaua kiungo kuimrisha foward

    ReplyDelete
  3. Kocha anajua afanye nini mechi na Azam huku akijua pia anapaswa kuwa na tahadhali gani mechi inayofuata na Vita Club. Sisi wapenzi tunajua la Azam tu. Tumuache yeye ndio mwisho wa siku anawajibika.

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic