KOCHA mkuu wa Simba Didier Gomes, ametamba kuwa, licha ya kuwaheshimu wapinzani wake katika mchezo wa kesho Tanzania Prisons, lakini anaamini kikosi chake kitaibuka na ushindi kwenye mchezo huo.
Simba inaingia katika mchezo huu ikiwa na kumbukumbu nzuri ya ushindi wa mabao 3-0 kwenye mchezo wao uliopita dhidi ya JKT Tanzania.
Akizungumzia mchezo dhidi ya Prisons Gomes
amesema:"Kikosi chetu kiko tayari kwa ajili ya mchezo wetu wa kesho dhidi
ya Tanzania Prisons, tunajua hautakuwa mchezo rahisi kutokana na uhalisia wa
timu ambayo tunakwenda kucheza nayo.
“Simba ilipoteza mchezo wa
mzunguko wa kwanza dhidi ya timu hii, na hivyo tunapaswa kuwa makini zaidi
dhidi yao kwani hiyo inaonyesha ni kwa kiasi gani wana timu ambayo inaweza
kupambana.
“Lakini matokeo ya ushindi katika
mchezo huu ni ya muhimu kwetu, tunapaswa kushinda ili kuendelea kuusogelea
zaidi uongozi wa ligi ambayo kwa sasa inashikiliwa na Yanga,”
0 COMMENTS:
Post a Comment