MAKAMU Mwenyekiti wa Kamati ya Mashindano ya Yanga, Injinia Hersi Said amesema kuwa wana mipango mirefu na Kocha Mkuu wa timu hiyo Cedric Kaze hivyo bado yupo ndani ya kikosi hicho.
Hivi karibuni kumekuwa na presha kubwa kwa Kaze kutajwa kuwa amepewa mechi kadhaa ili aweze kuchimbishwa kutokana na kuwa na mwendo ambao hauridhishi.
Taarifa zimekuwa zikieleza kwamba mabosi wa Yanga wapo kwenye mpango wa kumfuta kazi kocha huyo ili waweze kuleta kocha mpya.
Kwenye mechi za mzunguko wa pili baada ya kuongoza kwenye mechi nne ambapo amekuwa na mwendo wa kusuasua.
Alianza kwa sare ya kufungana bao 1-1 dhidi ya Tanzania Prisons, Uwanja wa Nelson Mandela, sare ya kufungana bao 1-1 dhidi ya Mbeya City na sare ya kufungana mabao 3-3 dhidi ya Kagera Sugar.
Ameshinda bao 1-0 dhidi ya Mtibwa Sugar na bao 1-0 dhidi ya Ken Gold kwenye mchezo wa Kombe la Shirikisho hatua ya 32 bora na timu hiyo imetinga hatua ya 16 bora.
Injinia ambaye ni Mkurugenzi wa Kampuni ya GSM ambao ni wadhami wa Klabu ya Yanga, amesema:"Kaze yupo ndani ya Yanga kwa muda mrefu kwa kuwa ni mwalimu ambaye tumemwamini na hakuna ambaye anafikiria kuachana naye.
"Kuna timu nyingi duniani ambazo zimekuwa zikipata matokeo mabovu ikiwa ni pamoja na ile ya Liverpool ambayo inanonolewa na Kocha Mkuu, Jurgen Klopp.
"Hivyo kupata matokeo mabovu haina maana kwamba Klopp ni mbovu, na timu yetu haijapata matokeo mabaya na haina matokeo mabovu kwa kuwa bado haijapoteza mechi yoyote ya ushindani," amesema.
Kwa sasa timu ipo Tanga na kesho ina kazi ya kusaka pointi tatu mbele ya Coastal Union, Uwanja wa Mkwakwani, Tanga.
Mzunguko wa kwanza Yanga ilishinda mabao 3-0 hivyo kesho kila timu itakuwa inahitaji kuweka rekodi yake, Yanga kulinda na Coastal Union kutibua.
Coastal piga hao vyura wapiteane jumla
ReplyDeleteWapoteane
ReplyDeleteKama timu haaina matokeo mabovu sasa huo mfano wa Klop na Liverpool unakujaje
ReplyDeleteLigi Bado sana kufukuza Coach sio solution ya kutibu matatizo, Big up kwa GSM wanajua wanachofanya ndio maana hawaendi kwa mihemko ya mikia
ReplyDeleteGSM au Yanga?Which is which?Nani sasa ana sauti ys kusema kuhusu kocha ?Mwenyekiti au GSM?
ReplyDeleteTumechukuliwa mateka na GSM wanayanga tuzibe midomo hatuna cha kufanya.
wewe unaleta fitna na sio shabiki wa Yanga
DeleteWew kama hayakuhusu pita kushoto
DeleteKazi wanay kwamaan kila mech wao wana cheza kwa presha
ReplyDeleteet liverpool, kwani hao Yanga walicheza vizuri misimu miwili iliopita mpaka mjilinganishe na liverpool??? akili ndogo
ReplyDeleteElewa kwanza ndipo ujibu usikurupuke huo ni mfano hajamanisha kwamba yanga na Liverpool ni sawa
DeleteHii ndo yanga bwana, ina misimamo yake sio kama unavyoropoka wew. Yanga tuendelee kusonga mbele
ReplyDeleteKaze hana muda mrefu atasepa
ReplyDeleteWewe kama sio mwana yanga usichangie kwani hayakuhusu
ReplyDeleteUamuzi wa kutofukuza kocha ni wa busara kwani tunapofikiria matokeo hasi tufikirie pia matokeo chanya. Suala hapa ni nani mweny kauli ya mwisho kati ya Yanga na GSM?
ReplyDelete