April 1, 2021


 
WAKATI uliopo kwa sasa kwa timu zote ambazo zinashiriki Ligi Kuu Bara, Ligi Daraja la Kwanza pamoja na Ligi ya Wanawake Tanzania ni kupiga hesabu za mwendo wao ambao wanakwenda nao.

Ukitazama kwa haraka kila timu inapoanza msimu imekuwa ikiweka malengo ila mwisho wa siku inakuwa ngumu kuona kama yametimia au la kwa kuwa hawana muda wa kuyatazama.

Ikiwa timu zitapata muda wa kujipanga upya itakuwa kazi rahisi kwa kila mmoja kufurahia mafanikio ambayo watayapata.

Kupitia mchakato wa kutazama kule ambako timu imetoka na ilipo inatoa taswira kamili ya kupata kile ambacho timu inahitaji kuwa nacho wakati ujao.

Kwa kufanya hivyo itatoa fursa ya timu kujua pale ambapo imekosea na kuanza upya pale ligi itakaporejea kwa kasi kwa kuwa mzunguko wa pili kila timu inapambana.

 


Tunapitia kwenye kipindi kigumu kwa sasa, ipo wazi ila ni somo kwamba hapa dunia kwetu ni njia na kila mmoja lazima ajiandae kwa ajili ya jambo hilo.

Kwa familia ya michezo imeona namna ambavyo kuondoka kwa aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, John Magufuli ametuacha Watanzania kwenye majonzi.

Muda ambao timu zitakuwa zinatafakari kuhusu kuanza maisha mapya bila uwepo wake ni muhimu pia kutazama yale ambayo yalikuwa yamepangwa kufanywa na timu husika.

Kupenda kwake michezo kulikuwa wazi kwa kila Mtanzania na wapenda michezo kwa kuwa alikuwa anajitoa na kutumia muda wake zama za uhai wake kuzungumza na wanamichezo.

Ni ngumu kwa timu kufikia malengo ambayo alikuwa anafikiria shujaa wetu Magufuli kwa kuwa yalikuwa ni maono makubwa ila lazima yafikiriwe kwa kila timu.

Ndoto yake kubwa ilikuwa siku moja aone timu ya Tanzania ilete ubingwa wa Afrika jambo ambalo halikukamilika mpaka anaondoka hivyo ni muhimu kila timu kupiga hesabu za pale ambapo zilikwama.

 

Ni Muda wa maandalizi unatumika kurekebisha makosa ambayo yanafanywa ndani ya uwanja. Kila mchezaji anajukumu la kufanya kazi yake kutimiza majukumu anayopewa.


Maandalizi ni muda huu na sio wakati wa kucheza mechi za ushindani. Muda ule huwa unakuwa maalumu kuweza kuona kile ambacho walikuwa wakifanya mazoezi.

Matokeo yanatafutwa kwa kila mmoja kufanya vizuri kuanzia kwenye maandalizi kabla ya mchezo wa ushindani.

Jambo kubwa la kufanya ni kukubali kujifunza na pale ambapo mnakosea mna kazi ya kurekebishana wenyewe kwa wenyewe ili kusaka matokeo kwenye mechi zenu ambazo mtacheza.

Kila mchezaji anapenda kuona timu inapata matokeo mazuri. Ikiwa morali itakuwa kubwa kwa kila mchezaji itaongeza nguvu pia ya kupata matokeo mazuri wakati ujao kwenye mechi za ushindani.

Imani yangu ni kwamba kila kitu kinawezekana. Ili kuweza kujiondoa kwenye ile presha ya kushuka daraja ama kukosa ubingwa ni muhimu kila mmoja kutimiza majukumu yake bila kusukumwa.

Zipo timu ambazo zinaiwakilisha Tanzania kwenye mashindano ya kimataifa nazo zina kazi ya kuweza kufanya vizuri na kutazama pale ambapo zilikuwa zimekosea awali.

Namungo FC ilikwama kwenye mechi zake zote mbili za kimataifa katika Kombe la Shirikisho, ile ya ugenini na nyumbani. Hakuna haja ya kukata tamaa muhimu kuangalia pale ambapo timu ilikosea.

Ikiwa wachezaji watakata tamaa muda huu wakati wa kupata matokeo chanya itakuwa ngumu kwa timu hiyo kushinda kwa sababu hakutakuwa na nguvu ya timu hizo kusaka ushindi.

Yote kwa yote ni jukumu letu kufanya yote kwa juhudi ili kupata matokeo mazuri ambayo ni furaha kwa mashabiki.

Na namna ambavyo timu itakuwa inapata matokeo itakuwa ni furaha pia kwa Watanzania wapenda michezo.

Simba ambayo inawakilisha nchi kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika ikumbuke kuwa ina kazi ya kusaka ubingwa wa Afrika na inawezekana ikiwa kutakuwa na mipango makini.

Kuongoza kundi haina maana kwamba imemaliza kazi hapana inajukumu la kusaka ushindi kwenye mechi zake zizilizobaki ili kufikia malengo.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic