SELEMANI Matola, Kocha Msaidizi wa Simba,
amesema kuwa wanapata tabu kupanga kikosi
cha kwanza kutokana na ubora wa wachezaji
wote walionao kikosini.
Simba ni mabingwa watetezi wa Ligi Kuu Bara
wakipambana na watani zao wa jadi, Yanga
ambao wapo nafasi ya kwanza na pointi zao 57 huku wao Simba wakiwa nafasi ya pili na pointi 55.
Akizungumza na Saleh Jembe, Matola
amesema kuwa kitu ambacho kinalichanganya
benchi la ufundi la Simba ni katika kupanga
kikosi cha kwanza.
“Tuna wachezaji wazuri ndani ya kikosi cha
Simba jambo hilo linatufanya tuwe tunapata
tabu kwenye kupanga kikosi cha kwanza, hii
inatokana na wachezaji wetu wote kuwa bora.
“Kuanzia Chama, (Clatous) Jonas (Mkude), Luis, (Miqiussone) John
(Bocco), Morrison (Bernard) hawa wote ni
wachezaji wazuri sasa wakati wa kupanga kikosi
cha kwanza huwa tunapata tabu na hili
linatuchanganya.
“Ila yote haya ni muhimu kuweza kufanya vizuri
kwa sababu ili uweze kupata matokeo mazuri ni
lazima uwe na kikosi kizuri na chenye wachezaji
bora, hicho ndicho kinachofanya tufanye
vizuri,” amesema Matola.
Mechi mbili wakiwa nje ya Dar wameweza kukusanya pointi sita na mabao matatu huku ngome yao ya ulinzi ikiwa haijaruhusu bao.
Ilishinda kwa tabu mbele ya Mwadui FC hii ni kwa mujibu wa Matola, pale ubao uliposoma Mwadui 0-1 Simba na Kagera Sugar 0-2 Simba.
0 COMMENTS:
Post a Comment