April 14, 2021

 



UONGOZI wa Klabu ya Yanga umeweomba mashabiki na wanachama wa Yanga kuwasilisha malalamiko yao kwa viongozi pale wanapobaini kuna tatizo.

Ofisa Habari wa Yanga, Hassan Bumbuli amesema kuwa tabia ya mashabiki kusema matatizo yao mitandaoni kila kitu hayaleti picha nzuri. 

Baada ya sare ya bao 1-1 dhidi ya KMC mashabiki wa Yanga walikuwa wakilalamika kwa kusema kuwa mwendo ambao wanakwenda nao hauwapi fuaraha zaidi ya stress.

Bumbuli amesema:-"Wanachama na mashabiki waache tabia ya kutaka umaarufu kwa kuzungumza,  kama wameona tatizo baada ya mechi waje klabuni kusema au watupigie simu maana wanazo namba zetu.

" Ukisema unawapa faida vyombo vya habari halafu wachezaji wanawachanganya safari ya ubingwa inahitaji uvumilivu,".


Kwenye msimamo wa ligi Yanga ina pointi 51 ikiwa nafasi ya kwanza baada ya kucheza mechi 24.

9 COMMENTS:

  1. Tutawapigia sana wao ndio wanacheza hovyo kabisa kama hawajala tutawapigia

    ReplyDelete
  2. Tunawaambia wajirekebishe mpira unachezwa hadharan tunaona madudu yote yanayofanyika

    ReplyDelete
  3. Simu zenu zinakuwa zimezimwa au ziko bize, heri niongee tu na chombo cha habari nitoe ya moyoni nikalale kwa unafuu kidogo

    ReplyDelete
  4. Tupige simu za nini na nyie hamtaki kubadilika. Hadi leo timu haina kocha wa maana. Mmekalia ubahili na hiyo gsm yenu. Angalieni wenzetu simba. Kocha safi uongozi safi ueekezaji safi mfumo safiii

    ReplyDelete
  5. Wanazingua sana wachezaji. Mashabiki tunakosa AMANI kabisa

    ReplyDelete
  6. Uwekezaji uko vizuri, shida ufundishaji mbovu mtu hajui hata mazoezi ya kuwongezea uwepesi wachezaji? Pili kamati ya ushindi sijui ipo au la, na kama ipo imelala usingizi.

    ReplyDelete
  7. Kwani wakiongea kwenye media ujumbe haufiki? Au kwani wao wanapofanya utopolo wao uwanjani huwa wanatupigia simu kuwa wanaenda kufanya utopolo

    ReplyDelete
  8. Ni kweli maneno ya mashabiki yanawachanganya wachezaji

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic