MSHAMBULIAJI wa kikosi cha Gwambina FC kinachonolewa na Kocha Mkuu, Badru Mohamed, Meshack Abraham amesema kuwa ofa zote ambazo amepewa kwa sasa ni lazima zisubiri mpaka msimu uishe kwa kuwa wanapambana kubaki ndani ya ligi.
Imekuwa ikielezwa Meshack Abraham anatazamwa
kwa ukaribu na Yanga pamoja na KMC ambazo zinahitaji kupata saini ya nyota huyo mwenye uhakika na namba
kikosi cha kwanza.
Meshack mwenye mabao 9 ndani ya ligi akiwa ni amesema kuwa anasubiri kwanza ligi iishe ndipo aweze kuzungumzia kuhusu ofa zake.
“Kwa wakati huu ofa zilizopo ngoja
tuzisubirishe kwanza kwa kuwa ligi bado inaendelea na sio wakati wa kuzungumzia
hayo hivyo acha kwanza tupambane itakuwa wazi.
“Ni kweli kuna timu ambazo zimeonyesha
nia ya kuhitaji huduma
yangu ila kwa sasa siwezi kuzitaja na sifikirii masuala hayo zaidi ya kuipa mafanikio timu yangu,” amesema.
Gwambina FC kwenye msimamo ipo nafasi ya 12 ina pointi 30 baada ya kucheza jumla ya mech1 27.
Mnyama ingilia kati hapo uvune awe mwenza wa Boko
ReplyDelete