July 18, 2021


 KIUNGO mshambuliaji wa Wydad Casablanca ya 
nchini Morocco, Simon Msuva, ameweka rekodi ya kuwa Mtanzania wa kwanza kubeba ubingwa wa ligi nchini humo, maarufu kwa jina la Botola Pro.


Nyota huyo amesema kuwa ilikuwa ni malengo yake kuona kwamba anaweza kutwaa ubingwa na timu hiyo.

Casablanca ilitangaza ubingwa huo baada ya kufanikiwa kuwafunga wapinzani wao Mouloudia Oujda mabao 2-0.


Msuva anaipa ubingwa huo Casablanca ukiwa ni msimu wake wa kwanza tangu ajiunge nao akitokea Difaa El Jadida ya nchini humo.


Ubingwa huo ni wa 21 ambao wameuchukua timu hiyo ambayo ilishiriki Ligi ya Mabingwa Afrika pia msimu huu.


Kiungo huyo ameweka rekodi kubwa ambayo

baadhi ya wachezaji waliowahi kucheza na

 wanaocheza akiwemo Nickson Kibabage

anayeichezea Club Athletic Youssoufia

Berrechid ya nchini humo, wamempongeza.


Akizungumzia ubingwa huo, Msuva alisema: “Ni

furaha kwangu kuweka historia yangu katika

maisha ya soka kuchukua ubingwa hapa

Morocco.


“Tangu najiunga na Casablanca haya yalikuwa

malengo yangu ya kwanza kubeba ubingwa wa

ligi kuu, licha ya kutamani zaidi kutwaa ubingwa

wa Ligi ya Mabingwa Afrika.”

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic