MZEE Maarufu kwa sasa kwenye ulimwengu wa michezo kutokana na maneno yake ya kibabe, Mzee Mpili amesema kuwa sababu kubwa ya ushindi mbele ya Simba.
Jana Uwanja wa Mkapa ubao ulisoma Simba 0-1 Yanga jambo lililowafanya mashabiki wa Yanga kusepa uwanjani na furaha huku mashabiki wa Simba wakiwa hawana jambo la kufanya wakati huo.
Hivi karibuni Mpili aliweka wazi kwamba hakuna namna ambayo Simba ingeweza kufanya mbele ya Yanga kwa kuwa kichapo kilikuwa hakiepukiki.
"Hamna namna lazima Simba ifungwe na mchezo wetu tutakapokutana kwa kuwa kikubwa ni kuona kwamba tunapata ushindi," alisema Mpili.
Mzee huyo ambaye maskani yake ni Ikwiriri mkoani Pwani amekuwa gumzo kwa sasa kwenye mitandao pamoja na kutajwa kwa mashabiki wa soka la Tanzania akitajwa kuwa nyota wa mchezo.
Mbwembwe tu hizo
ReplyDeleteUyu ndio aliesababisha goli lisionekane
ReplyDeleteSemeni ukweli tu kwamba jana paliumana kutumia "madawa ya kuongeza nguvu", bangi na kupuliza vyumbani, ndo maana wengi walionekana kama siyo wao
ReplyDeleteMzee mnampa kiki isiyo yake, ngoja trh ,25 tuwagonge
ReplyDeletewasubiri tarehe 25 watatujua tuu
ReplyDelete