July 25, 2021


 HATIMAYE Kamati ya Usajili ya Yanga,

inayoongozwa na Makamu Mwenyeikiti wake,

Eng. Hersi Said, imedaiwa kufanikiwa

kupenyeza ofa yao ya kumnasa kiungo

mshambuliaji wa Kaizer Chiefs ya Afrika Kusini,

raia wa Kenya, Anthon Akumu ili aje kurithi

mikoba ya Haruna Nyinzima.


Tangu Julai 15, mwaka huu, baada ya Yanga

kumuaga rasmi nyota Niyonzima ambaye ni raia

wa Rwanda, imefahamika wazi kuingia moja

kwa moja kwenye mawindo ya kupata mbadala

 wake, ambapo imegota kwa Athon Akumu,

anayeitumikia Kaizer.


Taarifa kutoka kwa mmoja wa viongozi wa timu

ya Kaizer Chiefs, Vina Maphosa, ameliambia

Championi Ijumaa kwamba, ni kweli amesikia

taarifa za Yanga kuleta ombi wakati yeye na

timu hiyo walikuwa nchini Morocco ambako

walienda kwa ajili ya Fainali ya Kombe la

Mabingwa Afrika.


“Kuhusu suala la Yanga kumhitaji Akumu, kwa

sasa mimi siwezi sana kulielezea maana ndiyo

nimetua muda si mrefu nikitokea Morocco,

ambapo nilienda kwa ajili ya mchezo wetu na Al

Ahly, hivyo nitakuwa na mapumziko kwa

takriban siku tano.


“Zaidi nikuombe uwe mvumilivu maana nitajua

hilo suala baada ya kuingia kazini kuanzia

Jumatatu ya Julai 26, mwaka huu, hapo sasa

nitakuwa na majibu ya wazi juu ya jambo hilo,”

alisema Maphosa.



1 COMMENTS:

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic