July 16, 2021


 KLABU ya Yanga imeonyesha heshima kwa kuamua kutoa mkono wa byebye kwa nyota wake, Haruna Hakizimana Niyonzima raia wa Rwanda.


Niyonzima ameagwa kwa heshima wakati Yanga ikiivaa Ihefu FC iliyokuwa inapambana kuhakikisha inashinda mechi yake dhidi ya Yanga ili ibaki Ligi Kuu Bara.

Yanga wameamua kumuaga Niyonzima kutokana na kazi kubwa aliyoifanya akiwa na kikosi cha Yanga ambacho kimemaliza msimu kikiwa katika nafasi ya pili lakini kimetinga fainali ya Kombe la Shirikisho la Azam Sports.

Kiungo huyo amefanya mengi makubwa akiwa na kikosi cha Yanga, pamoja na kwamba alilazimika kuondoka mara moja na kurejea tena.

Mara moja, Niyonzima aliondoka na kujiunga na watani wa Yanga, Simba ambako baada ya hapo aliondoka na kwenda zake kwao Rwanda.

Wakati Yanga wakipika kikosi upya walimfuata tena Kigali ambako walizungumza naye na kufanikiwa kumrejesha. Amekuwa na mchango wake wakimaliza nafasi ya pili na fainali ya Kombe la Shirikisho.

Pamoja na yote, Niyonzima ameacha alama wakati wa ile Yanga ya Kampakampa tena ambayo ilikuwa ikitoa mateso kwa watani wake Simba kila mara.

Yanga ambayo ilikuwa ni burudani ya aina yake na kama unakumbuka, wakati anaingia pacha kwenye kiungo alikuwa ni Athuman Iddi Chuji na wakatikisa hasa. Wakati Chuji anaondoka Yanga, Niyonzima aliendelea kutamba na kwa wakati mwingine tena akasumbua akiwa na Thabani Kamusoko, wakiifanya Yanga kuwa gumzo hadi inatinga hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika.


Bila shaka Yanga wanafanya jambo bora

kabisa la kumuaga raia huyo wa Rwanda

kutokana na kazi yake nzuri aliyoifanya

akiwa na Yanga kwa vipindi hivyo viwili

na anakuwa mmoja wa wachezaji wa

kigeni waliofanya vizuri zaidi katika Ligi

Kuu Bara.


Sasa anaondoka, heshima anastahili na

mimi ninauga mkono ingawa nina jambo

la kuuliza. Kwamba huu utaratibu mara

kadhaa, kuanzia kwa Yanga na baadhi ya

klabu zimekuwa zikiona sahihi kuwapa

heshima kwa kuwaaga au kuwapongeza

wachezaji wanapokuwa wanaondoka na

zaidi ni wale wa kigeni.



Kwa Yanga, inaweza kuwa imefanya kwa

wazalendo, lakini nawauliza tena,

hawaoni wachezaji kama Kelvin Yondani

pia walipaswa kuagwa kutokana na

mchango wao.


Mfano, wakati akiondoka Niyonzima,

ninaamini Yondani angekuwa tayari

ameishaagwa. Wakati fulani alikaa nje

bila ya timu na Yanga ilimaliza msimu

ambapo ingeweza kufanya jambo kwake

na kumuaga kwa kuwa alikuwa anastahili

kuagwa ili kuonyesha wanajali muda

wote wa mafanikio akiwa Yanga.


Wakati Niyonzima akitamba akiwa na

Chuji, Kamusoko na wengine. Yondani

ndiye alikuwa akishikilia jahazi la ulinzi la

kikosi cha Yanga. Tena alifanya kazi bora

akiwa na Nadir Haroub ‘Cannavaro’,

lakini hata baada ya kustaafu kwake,

Yondani aliendelea kupambana akiwa na

wachezaji kadha wa kadha mfano wa


Vicent Andrew ‘Dante’, Shaibu Ninja,

Said Makapu na wengine, akaendelea

kuwa tegemeo na mhimili wa ulinzi wa

klabu ya Yanga.


Hata wakati ule Niyonzima alipoondoka

kwenda kwao Rwanda, Yondani alikuwa

bado anaitumikia Yanga. Niyonzima

aliporejea na kujiunga na Simba, Yondani

bado alikuwa akipambana kukitumikia

kikosi cha Yanga. Leo kwenye kuagwa,

hakuwahi kupewa hiyo heshima.


Vizuri kufanya kama hicho kilichofanyika

kwa Niyonzima lakini vizuri zaidi

kuwakubuka waliofanya vizuri na kujituma kwa moyo wao wote kuhakikisha Yanga inapata inachotaka.

Tumeona hata Yanga mpya ambayo

ilibadili zaidi ya wachezaji 15, bado

haijafikia mafanikio ya waliyokuwa nayo

katika Yanga ya kina Yondani.


 Kama ambavyo nimekuwa nikisema siku zote,

timu inapaswa kuendelea kujengwa na

msimu ujao unaweza kuwa bora zaidi

kwa Yanga kama watajipanga lakini

naendelea kuwakumbusha, Yondani ni

gwiji nchini, ni mmoja wa wachezaji bora

wazalendo kuwahi kutokea nchini na

anapaswa kupewa heshima yake.


Inawezekana isiwe kwa Yondani pekee

au Yanga pekee, nizikumbushe klabu nyingine, kuwaaga wachezaji wao kwa heshima na hasa wale waliojituma hasa kutaka klabu iwe bora na kushinda, wanapaswa kupewa heshima zao na

tusiwadharau kwa uzalendo wao na mara nyingi nimeona, wako viongozi wengi katika klabu zetu wana hisia za kuwadharau wachezaji wazalendo kwa

kuwa tu, wanaona kuwafanya waonekane wakubwa ni kama wao viongozi kujishusha.


Tena wakati mwingine, unakuta kiongozi

ana miaka miwili tu ndani ya klabu lakini

mchezaji ameitumikia klabu kwa zaidi ya

miaka sita hadi nane. Huu si uungwana

na haifai kuendelea, badilikeni.

16 COMMENTS:

  1. Hebu tufafanulie zaidi katika hili,hivi ikitokea mfanyakazi wako akaamua kuondoka katika kampuni yako akaenda kampuni nyingine halafu akaamua kustaafu akiwa katika kampuni aliyohamia baada ya kutoka kwako je utafanya hafla ya kumuaga kwa kustaafu kwake?

    ReplyDelete
  2. Au kama huyo mfanyakazi aliondoka kwako akaenda sehemu nyingine na akawa anaendelea na kazi huko alipo je utalazimisha kumfanyia sherehe ya kustaafu? Au ulimaanisha send off?

    ReplyDelete
    Replies
    1. Kumbe niyonzima amestaafu?

      Delete
    2. Kwani wewe ulielewa nini katika kumuaga Niyonzima?Inaonesha una kamasi kichwani badala ya ubongo.Neno kustaafu unalitafsiri vipi?

      Delete
    3. Kamasi wanazo Utopolo maana mpaka leo wanaamini tar 23 watatangazwa mabingwa

      Delete
  3. Yondani hakupewa heshima yeyote pale yanga. Na hii ni kama vile hawakuona mchango wake zaidi ya maslahi yao kutimizwa. Baada ya Yondani kushindwana na yanga kwasababu ya maslahi na akakaa msimu mzima bila timu Yanga walijenga mtima nyongo badala ya kumuaga kwa mema aliyofanya akiwa nao. Hii sio sawa ni udanzwi mtupu

    ReplyDelete
    Replies
    1. Nyie mliwahi kumuaga nani ambae aliondoka kwa zengwe

      Delete
  4. Kwa kweli ni nani aliyeitumikia Yanga kwa kila mapenzi na uaminifu na kuipa mafanikio makubwa baina ya Niyonzima na Yondani?

    ReplyDelete
    Replies
    1. Yaani pamoja na kuihujumu timu yeye na kundi lake bado kuna nguchiro fulani wanataka tumpigie makofi

      Delete
    2. Mlichoma jezi ya Niyonzima alivyoenda Simba na mkamuita msaliti...msijasahaulishe bhana

      Delete
    3. Mbona mnateseka na timu sio yenu

      Delete
  5. Kila kitabu na zama zake! Kila jambo lina mwanzo

    ReplyDelete
  6. Mtoa posti acha uchochezi, ama vipi waulize Simba kwanini hawajamuaga Ibrahim Ajibu.

    ReplyDelete
  7. We Saleh tumia akili hatahizo kidogo ulizonazo.kelvin aligoma kusaini yanga wanamuaga vipi? Au umezoea kuhongwa ili uchonganishe washabiki?acha uandishi wakijinga ishu ikowazi wenye akiliwote wameelewa Ila vilaza Kama wewe ni mtihani.,Hunajipya kaa kumya

    ReplyDelete
  8. Yondani hajaondoka kwa maelewano mazuri, pia ukumbuke tim ilikua inapita ktk kipindi cha mpito.

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic