KIKOSI cha Yanga, leo kimeibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Simba inayonolewa na Kocha Mkuu, Didier Gomes.
Mchezo wa leo ambapo Simba ilikuwa inahitaji pointi tatu ili kutangazwa kuwa mabingwa wa Ligi Kuu Bara mambo yalikuwa magumu kwa timu hiyo iliyoshuhudia pointi tatu zikienda Yanga.
Ni Zawadi Mauya ambaye alikuwa shujaa wa mchezo wa jana kwa kupachika bao moja mbele ya Rais wa Tanzania, Samia Suluhu na kuwafanya Simba wasiamini wanachokiona.
Ushindi huo unaifanya Yanga kufikisha jumla ya pointi 70 ikiwa nafasi ya pili huku Simba ikibakiwa na pointi 73 baada ya kucheza jumla ya mechi 30.
Manara waandishi wakimpigia atakuwa mwehu
ReplyDeleteNdio Tabu ya kwenda na matokeo mfukoni, poleni watani
ReplyDeleteTabu iko wapi
DeleteHamkuiyona kweli au utani jamani
DeleteTumeshinda ingawa Simba walijitahidi kipindi cha pili. Kazi safi Yanga
ReplyDeleteYanga ijitahidi katika mechi mbili zilizobaki washinde huku wakiiombea Simba ipoteze zote 4 zilizobaki. Hakuna ajabu yo yote hapo
DeleteTumewalaani,wanapoteza zote hao.
ReplyDeleteKumpiga mtani raha yake zaidi ya kuchukua kombe,
ReplyDeleteHata wao lenho lao ilikua kuwapiga Yanga ilikuwatambia kibao kimegeuka
Siwaoni wale waliokuwa wanatukana kuhusu yanga au hawajatoka uwanjani hadi sasa
ReplyDeleteHakuna furaha kama furaha ya ubingwa kwahivo kamilisha furaha kwa kuuchukuwa ubingwa sio bao moja la nusuranusura
ReplyDelete