October 6, 2021


LEO Oktoba 6 Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania, (TFF) limemtambulisha Mdhamini Mkuu wa Ligi Kuu Tanzania Bara ambaye ni beki ya NBC.

Sasa ni rasmi Ligi Kuu Tanzania itafahamika kwa jina la NBC Premier League baada ya kusaini mkataba na TFF wenye thamani ya bilioni 2.5.

Ni Rais wa TFF, Wallace Karia amesaini dili hilo na Mkurugenzi wa NBC Theobald Sabi naye alisaini kwa upande wa NBC.

Kwa sasa Ligi Kuu Bara itakuwa inaitwa NBC Premier League kwa kuwa ni wadhamini wakuu.

Karia amesema kuwa miongoni mwa mchanganuo wa fedha hizo ni pamoja na kuutumia kwenye usafiri.

"Wakati wadhamini wa kwanza wanaingia wa ligi kuu madhumuni makubwa ilikuwa ni kusaidia usafiri wa timu kwenda kituo kingine kucheza mechi zake na hakukuwa na tatizo tena la timu kushindwa kufika kwenye kituo kwa sababu za kushindwa kumudu gharama za usafiri.


"Sisi kama TFF hatujabadili kitu sehemu kubwa ya hela hii itakwenda kwenye klabu kwa ajili ya kuwa sehemu ya usafiri sehemu ya mshahara tayari ishakuwa Coverd,".


5 COMMENTS:

  1. Kuna watu wanaoishi kizamani wataanzisha zogo la rangi za logo ya mdhamini. Next time watafute mdhamini mwenye rangi zao ili tupunguze mapovu. Najua timu nyingine hazina huo ujinga.

    ReplyDelete
  2. hatumkatai mdhamini lakini hatutaweza kuvaa hiyo rangi......so hatujawahi kutaka ujinga na hatutoutaka,hakuna namna NBC inabidi wawe wapole tu watubadilishie hiyo rangi kwenye jezi zetu.

    ReplyDelete
  3. Bado mnaishi karne ya ujima, imani potofu kibao, badilikeni

    ReplyDelete
  4. Very simple hasiyetaka basi yeye adhamini ligi au ajitoe, simple kabsaa,

    ReplyDelete
  5. Plot 89 block 25 makao makuu majengo usongo Olympic lran inashindana.

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic