October 1, 2021


FT:Uwanja wa Jamhuri, Dodoma Simba inasepa na pointi tatu mbele ya Dodoma Jiji ikiwa ni mchezo wa pili kwenye ligi na wanakusanya pointi na kufunga bao kwa mara ya kwanza.

Kipindi cha pili

Dodoma Jiji 0-1 Simba

Zinaongezwa dakika 5

Dakika 90 Bwalya kwake Bocco ni zamu ya Dilunga anachezewa faulo

Dakika ya 89 Inonga kwake Bocco, Mzamiru kwake Bwalya kisha ni zamu ya Inonga kuelekea Dodoma Jiji ni Kibacha anaokoa majalo

Dakika ya 88 Mzamiru Yassin anafanya jaribio akiwa nje ya 18 lnakwenda juu ya lango

Dakika ya 87 Masalanga anaokoa hatari kwenye lango lake na kuanzisha kuelekea kwa Simba

Dakika ya 86, Dilunga kwake Meddie, Bwalya kwake Nyoni mlinda mlango Masalanga anainyaka

Dakika ya 84 Simba wanapeleka mashambulizi kwa Dodoma Jiji kupitia kwa Mugalu

Dakika ya 77 Manula anapewa huduma ya kwanza baada ya kuchezewa faulo na mchezaji wa Dodoma Jiji ambaye alionyeshwa kadi ya njano

Dakika ya 69 Kagere anafunga goooooooal kwa pasi ya Mugalu ya kichwa akiwa ndani ya 18.

Dakika ya 63, Lwanga anatoka anaingia Kagere, anatoka Mhilu anaingia Duncan Nyoni, Tshabalala anafanya jaribio linaokolewa 

Dakika ya 59 Salmin Hoza anaonyeshwa kadi ya njano kwa kumchezea faulo Lwanga

Dakika ya 58 Mkandala anapeleka mashambulizi kwa Simba inaokolewa na Manula

Dakika ya 57 Dodoma Jiji wanapeleka mashambulizi Simba 

Dakika ya 56 Bocco anatoa mpira nje

Dakika ya 54 kona ya kwanza kwa Simba inapigwa na Bwalya 

Dakika ya 52 Karihe anaingia anatoka Mcha, anafanya jaribio kali nje ya 18 linaokolewa na Manula karibu na Joseph Akamba ambaye ni mwamuzi wa kati

Dakika ya 51 Masalanga anaanzisha mashambulizi kwenda Simba

Dakika ya 50 Dodoma Jiji wanapeleka mashambulizi Simba, Inonga anaokoa

Dakika ya 46 Bocco anafanya jaribio la kwanza linakwenda juu ya lango 

Dakika ya 45 John Bocco anaingia anatoka Mwenda

Kipindi cha pili kimeanza 

Mapumziko 


Dodoma Jiji 0-0 Simba

Dakika ya 45 Inonga anaingia anatoka Kenedy Juma 

Dakika ya 44 Anuary Jabir anaonyeshwa kadi nyekundu kwa kumchezea faulo Kenedy Juma 


Dakika ya 40 Kenedy Juma anapewa huduma ya kwanza baada ya kugongana na mchezaji wa Dodoma Jiji


Dakika ya 38 Mkandala anafanya jaribio akiwa nje ya 18 linakwenda nje
Dakika ya 37 Mhilu anapiga shuti akiwa nje ya 18 linakwenda nje ya lango
Dakika ya 36 Khamis Mcha anachezewa faulo na Mwenda 
Dakika ya 34 Dilunga anachezewa faulo, Bwalya anajaza majalo yanakwenda mazima nje
Dakika ya 32 Mugalu anacheza faulo akiwa ndani ya 18 
Dakika ya 31 Lwanga anachezewa faulo
Dakika ya 30 Dilunga anachezewa faulo na Mkandala
Dakika ya 29 Mhilu anaotea kwa mujibu wa mwamuzi
Dakika ya 27 Manula anapeleka mashambulizi Dodoma Jiji 
Dakika ya 25 Wawa anasababisha kona inapigwa na Jamal Tegeta inaokolewa na wachezaji wa Simba wanapata kona nyingine Dodoma Jiji inapigwa na Khamis Mcha kichwa cha Ngalema kinakwenda nje
Dakika ya 23 Wawa anaanua majalo yanayomfuata Manula, Dodoma Jiji wanapeleka mashambulizi Simba, Mwenda anaokoa
Dakika ya 22 Masalanga anaanzisha mashambulizi kwenda Simba, Mugalu anacheza faulo
Dakika ya 21 Bwalya anapiga faulo inaokolewa
Dakika ya 20 Simba wanapata faulo
Dakika ya 19 Mkandala anapeleka mashambulizi Simba a apokwa mpira na Mugalu anafanya jaribio linakwenda nje ya lango. 
Dakika ya 18 Dodoma Jiji wanapeleka mashambulizi Simba
Dakika ya 17 Dilunga anachezewa faulo 
Dakika ya 16 Dodoma Jiji wanapeleka mashambulizi Simba
Dakika ya 14 Simba wanapiga faulo baada ya Khamis Mcha kucheza faulo na Mugalu anamchezea faulo kipa wa Dodoma Jiji Masalanga.
Dakika ya 13 Mwenda anapiga faulo inakwenda nje pia anaingia Bwalya kuchukua nafasi ya Sakho
Dakika ya 12 Sakho anatolewa akiwa amebebwa kwenye machela
Dakika ya 11 Mwenda anachezewa faulo
Dakika ya 9 Mwenda anapiga faulo inaokolewa na kipa wa Dodoma Jiji 
Dakika ya 7 Sakho anapewa huduma ya kwanza
Dakika ya 6 Wawa anapeleka majalo mbele, Mzamiru anakata umeme kwa Ngalema
Dakika ya 4 Mzamiru Yassin anapewa huduma ya kwanza
Dakika ya 3 Dodoma Jiji mwendo wa pasi fupifupi kulifuata lango la Simba
Dakika ya 2 Dilunga anachezewa faulo
Uwanja wa Jamhuri,  Dodoma


Dodoma Jiji 0-0 Simba

10 COMMENTS:

  1. Dereva msaada kwenye tuta!!!!!!

    ReplyDelete
  2. Mtateseka sana na ngoja tupate first eleven na huyo zeruzeru wenu,tunachukua mara tano mfululizo ili mjitoe vizuri kwenye league

    ReplyDelete
    Replies
    1. Mshapigwa changa la macho...hehehe

      Delete
  3. Kikosi kipana kimekuwa cha kutafuta first eleven tena?

    ReplyDelete
  4. Mnatoa hela tuumiziwe wachezaji, huo ufala.

    ReplyDelete
    Replies
    1. Safari hii hamna za kupenyeza sio? Wajitegemee ndio kazi yao.

      Delete
  5. Simba imepeleka wachezaji 9 kwenye timu ya Taifa, hilo linaonekana kuwaumiza wengine.

    ReplyDelete
    Replies
    1. Kwa viwango vya bongo..sisi tuko professional zaidi

      Delete
    2. Professional ya nini labda??mngepigwa na rivers nje ndani??mnajitoa ufahamu mmepigwa jumla ya mechi tatu,zanaco,na mkapigwa na rivers kwa mkapa na mkapigwa tena nigeria,wakati simba kapigwa mechi mbili ambazo ni ya mtani na na mazembe ila ninyi mnajifanya kujitoa ufahamu kwelikweli poleni sana,endeleen kusubiri meli airport atashuka rubani utasema nahodha.poleni sana.

      Delete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic