September 16, 2014

Nahodha wa Liverpool, Steven Gerrard ametamba kwamba wamerudi kazini kwenye Ligi Kuu ya Mabingwa Ulaya..

Mara ya mwisho Liverpool ilicheza michuano hiyo mikubwa zaidi kwa ngazi ya klabu mwaka 2009.
Gerrard amesema alikuwa akiumia na kujisikia vibaya lakini hakuwa na namna. Hivyo watafanya kila linalowezekana kufika mbali.
Mara ya mwisho Liverpool ilitwaa kombe hilo mwaka 2005 katika mechi iliyopigwa Istambul Uturuki dhidi ya AC Milan ya Italia.
Gerrard amecheza mechi 129 za mechi za Ulaya zilizo chini ya Shirikisho la Soka Tanzania (Uefa) wakati wachezaji wengine wote waliobaki kwenye kikosi hicho ukijumlisha mechi zao za kimataifa wakiwa na Liverpool zinafikia 153.

Aidha, Gerrard amewaambia watu ambao wamekuwa wakimuita mshambuliaji Mario Balotelli kuwa ni mtu wa hovyo, wao wala hawajali.
"Wamuite wanavyotaka kwa kuwa wanaona sawa, sisi hatubabaiki wala kujali hilo kwa kuwa tunajua Balotelli sasa ni mmoja kati yetu," anasema Gerrard akionyesha kujiamini. 

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic