September 15, 2016

Wakati pambano la timu ya Mwadui dhidi ya Yanga likizidi kupamba moto, Kocha Mkuu wa Mwadui ya mkoani Shinyanga, Jamhuri Kihwelo ‘Julio’ amesema atahakikisha anashinda mchezo wake dhidi ya wapinzani wake hao keshokutwa Jumamosi kwenye Uwanja wa Kambarage mkoani humo.

Kocha Julio amesema kuwa kutokana na yeye kutangaza kustaafu soka mara baada ya msimu huu kumalizika atahakikisha kuwa anaifunga Yanga ili astaafu soka kwa heshima, kitu ambacho kinaweza kuwapa hasira zaidi Yanga kuelekea mchezo huo.





“Nimejipanga kuhakikisha kuwa Yanga wanapata kipigo na nitahakikisha kuwa tunawapa kipigo kikali ili watambue kuwa makocha wazawa ni wazuri kuliko Wazungu.

“Ifahamike tangu timu yangu ipande daraja Yanga haijawahi kunifunga kwenye uwanja wa nyumbani hivyo sitaruhusu historia ivunjwe bali nitahakikisha kuwa Yanga haondoki na pointi katika mchezo huo.

“Mimi sitishwi na ubora wa wachezaji wa Yanga bali nitahakikisha malengo niliyojiwekea yanatimia kwani kila mchezaji wangu nimempa majukumu maalumu ya kuhakikisha kuwa wachezaji wa Yanga hawaleti madhara kwenye lango letu hivyo lazima walifahamu hilo,” alisema Julio.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic