September 15, 2016

Kikosi cha Yanga kimeondoka alfajiri ya leo jijini Dar es Salaam kuelekea Mwanza kisha Shinyanga kwa ajili ya mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya Mwadui FC.


 







Yanga na Mwadui zanatarajiwa kukutana Jumamosi ya keshokutwa kwenye Uwanja wa Kambarage mkoani Shinyanga, mchezo ambao unatarajiwa kuwa mgumu kutokana na upinzani wa timu hizo licha ya kuwa Yanga ndiyo ambayo inaonekana kuwa vizuri zaidi uwanjani kutokana na matokeo yake ya hivi karibuni.

Yanga iliondoka Dar es Salaam kwa ndege ya Fast Jet na tayari imetua Mwanza ambapo asubuhi hii ilikuwa ikifanya mchakato wa kuelekea Shinyanga.

Mwadui inanolewa na Kocha Jamhuri Kihwelo ‘Julio’ ambaye tayari amesikika akijinadi kuwa lazima ataifanyia Yanga kwa kuifunga na kuwataka wale wanaodhani kuwa mabingwa hao watetezi wa Ligi kuu Bara watapata pointi tatu kirahisi mkoani humo, wanajidanganya.

Mwadui ipo katika nafasi ya 11 kwenye msimamo wa ligi hiyo ikiwa na pointi 4 katika michezo minne wakati Yanga ina pinti saba katika michezo mitatu.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic