September 15, 2016

Katika kile kinachoonekana presha kuwa kubwa kuelekea mechi dhidi ya Simba, wikiendi hii, benchi la ufundi la Azam FC ambalo linaongozwa na makocha kutoka Hispania limekataa mazoezi yao kushuhudiwa na waandishi wa habari.

Leo asubuhi ikiwa ni siku mbili kabla ya mchezo huo ripota wa SALEHJEMBE alifika kwenye Uwanja wa Azam Complex kwa ajili ya kushuhudia kilichokuwa kikiendelea lakini akakutana na ukuta wa chuma.








Baada ya kufika uwanjani hapo aripota huyo aliambiwa hataruhusiwa kuingia ndani kushuhudia mazoezi hayo kwa kuwa tayari kocha ameanza mazoezi maalum kwa ajili ya mchezo huo wa Jumamosi hii kwenye Uwanja wa Uhuru.

Imeelezwa kuwa kocha huyo aliwakubalia watu wa habari wa klabu hiyo pekee lakini wengine wote kutoka nje ya Azam FC hawakuruhusiwa kushuhudia kilichokuwa kikiendelea.

Mchezo huo ni mmoja wa mchezo mkubwa kwa kuwa Azam imekuwa ikitoa ushindani mkali katika miaka ya hivi karibuni tofauti na zamani ambapo ilionekana mechi kubwa ni za Yanga na Simba pekee.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic