Askari Polisi wa Catalan wanakotokea Barcelona,
wametoa mpya ya mwaka baada ya kufanya jitihada kubwa ili kupata jezi na bukta
chafu za wachezaji wa Real Madrid.
Askari Polisi hao maarufu kama Mossos d'Esquadra,
walibaki kwenye milango kwenye uwanja wa ndege wakati Real Madrid wakiondoka
mjini hapo kurejea kwao baada ya ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Barcelona kwenye
Uwanja wa Camp Nou.
Kwa kuwa askari hao ndiyo walipewa kazi ya
kuhakikisha Madrid wanakuwa salama hadi watakapoondoka kwenye uwanja huo wa
ndege, waliitumia nafasi hiyo kuomba vifaa hivyo ambavyo walivitumia katika
mechi hiyo.
Pamoja na kujulikana wengi wao ni mashabiki wa
Barcelona, lakini walitumia muda wao mwingi kumpongeza Jose Mourinho na
wachezaji wake kwa ushindi huo mkubwa ambao umeonekana kama aibu kwa Barcelona.
Wachezaji wengi wa Madrid walikuwa wakiendelea na
sherehe, tokea siku iliyopita ambayo walishinda mechi hiyo hadi kesho yake
wakiwa wanaondoka kurejea Madrid.
Tayari Madrid imeanza kujiandaa na mechi inayofuata
dhidi ya Barcelona ambayo lazima watatakiwa kushinda bila ya kujali ugenini ili
kufuta aibu iliyowakuta katika mechi ya Kombe la Mfalme ambayo sasa wametolewa
na Madrid wametinga fainali na tayari wanajua watawavaa wapinzani wao wakubwa
Atletico Madrid katika fainali.
0 COMMENTS:
Post a Comment