Baada ya mashabiki kuendelea
kumsakama mfululizo, Kocha Mkuu wa Chelsea, Rafa Benitez ameamua kuwatolea
uvivu mashabiki wa Chelsea na ‘kuwaangushia’ mbofumbofu.
Benitez amewaambia mashabiki wa
Chelsea ni watu wa ajabu ambao wanaishambulia timu yao bila ya kujali lolotea.
Amesema anashangazwa na mashabiki
hao ambao wamekuwa wanamshambulia tokea alipochukua timu Novemba mwaka jana
bila ya kujali maendeleo ya timu.
“Sijawahi kuona mashabiki wa
namna hii, badala ya kujiandaa kuja kushangilia timu wanapoteza muda
kutengeneza mabango ya kunishambulia na kuisakama timu.
“Niko katika soka kwa miaka 26
sasa, nimebeba ligi ya mabingwa, Kombe la FA, Italia Super Cup na Ubingwa wa
Hispania mara mbili. Vipi leo naonekana kama kocha ninayeanza kazi.
“Wanasababisha presha kubwa kwa
mashabiki, hawawezi kutulia tena. Wakiendelea hivi, mwisho mwakani timu
itacheza Kombe la Europa kwa kuwa wachezaji wanakuwa hawajiamini,” alisema
Benitez.
Mashabiki wamekuwa wakimsakama
Benitez tokea achukue timu hiyo wakionyesha kutokubaliana na kuondolewa na Di Matteo.
0 COMMENTS:
Post a Comment