Wakati
mjadala wa chenga kali aliyompiga nahodha wa Barcelona, Cares Puyol kabla ya
kusababisha bao la pili wakati Real Madrid ikiishinda kwa mabao 3-1, sasa Angel
Di Maria ataikosa mechi nyingine ya El Classico.
Zinapokutana
Real Madrid na Barcelona ndiyo El Classico, mechi ijayo ni kesho Jumamosi na Di
Maria hatacheza kutokana na kulambwa kadi nyekundu baada ya njano mbili katika
mechi ya mwisho ya La Liga, pale timu yake ilipoivaa Deportivo la Coruna.
Madrid
imefanya kazi ya kukataa rufaa ili Di Maria acheze mechi hiyo, lakini imegonga
mwamba na kadi mbili njano za mwamuzi Álvarez Izquierdo, moja ikiwa ni ya
kuutupa mpira kwa hasira ya pili kukaa mbele ya ukuta pamoja na kuelekezwa na
mwamuzi, zimeonekana ni sahihi.
Huenda
Jose Mourinho akaamua kuanza na Mbrazil, Kaka katika nafasi hiyo ili kuendelea
kuipa presha Barcelona ambayo itakuwa imepania kulipa kisasi.
0 COMMENTS:
Post a Comment