Pamoja na kuendelea kuwa tishio
msimu huu na uliopita, imeelezwa kiungo nyota wa Tottenham Hotspur, Garreth
Bale amekuwa akivaa soksi maalum uwanjani.
Soksi anazovaa Bale zinajulikana
kwa jina la Trusox na zinatengenezwa nchini Marekani, kwa kiasi kikubwa ndizo
zinamuongezea kazi.
Soksi hizo zinaelezwa kumsaidia
mchezaji kutopoteza nguvu hata kidogo, badala ya kuongeza mwendo.
Kitu Kingine, soksi hizo ambazo
bei yake ni pauni 25 (Sh 63,750) ni bora kwa kulinda kifundo cha mguu maarufu
kama enka.
Kwa wachezaji wenye kasi kama
Bale, soksi hizo zimekuwa ni msaada mkubwa kwani kasi ya wachezaji kuzitumia
imekuwa ikiongezeka.
Wengine ambao wanatumia soksi
hizo ni pamoja na Demba Ba na Victor Moses raia wa Senegal na Nigeria
wanaokipiga katika klabu ya Chelsea ya London.
0 COMMENTS:
Post a Comment