Tokea
ameachwa Man United, mshambuliaji Dimitar Berbatov wa Fulham amekuwa akionyesha
uwezo mkubwa wa kupachika mabao.
Raia huyo
wa Bulgaria, pamoja na uwezo soka, hivi karibuni amewashangaza watu wengi baada
ya kuonyesha ana uwezo mkubwa sana uchoraji.
Hakuna
ubishi picha alizochora kutumia kalamu ya mkaa, Berbatov ameonyesha uwezo
mkubwa ikiwa ni pamoja na kuwachora watu wengi nyota duniani.
Pamoja na
kuwachora watu wanaohusika na mambo mbalimbali, lakini ameonyesha ni shabiki wa
miondoko ya hip hop baada ya kuwachora wakali wawili wa miondoko hiyo marehemu
2Pac Shakur na Snoopy Dogg Doggy.
Pia amethibitisha
yeye ni shabiki wa filamu za kibabe, baada ya kumchora Bruce Wills, mmoja wa
waigizaji wa Hollywood anayesifika kwa kuigiza filamu za aina hiyo.
Berbatov aliziweka picha hizo katika ukurasa
wake wa mtandao wa kijamii wa Facebook huku kukiwa na picha yake inayoonyesha
akiwa na kalamu hiyo ya mkaa sikioni.
0 COMMENTS:
Post a Comment