Viungo
Athuman Iddi ‘Chuji’na Haruna Niyonzima wataanza kazi ya kupiga mipira ya faulo katika mechi kati ya
Yanga dhidi ya Kagera Sugar kwenye Uwanja wa Taifa, Dar.
Kocha
Mkuu, Ernie Brandts amesema tayari walianza mazoezi kwa siku kadhaa na
wachezaji wanne watakuwa wakifanya kazi hiyo.
Pamoja na
Chuji na Niyonzima wengine ni mabeki Mbuyu Twite na Oscar Joshua.
Chuji na
Niyonzima watapiga faulo zote zinazotakiwa kupigwa kwa mguu wa kulia, huku
Oscar na Mbuyu watafanya kazi hiyo watakapopata faulo za mguu wa kulia.
“Katika mechi
ya leo, iwapo faulo zitatokea, jukumu litakuwa ni lao na watakachofanya ni
kujadiliana na mwisho ni kutumia uwezo wao na mafunzo waliyipata,” alisema
Brandts.
Mechi ya
leo ni muhimu sana kwa Yanga ambayo inahitaji ushindi ili kufikisha pointi 42
wakati Kagera yenye pointi 27 katika nafasi ya tano, inataka kupanda juu kwa
kupata pointi tatu muhimu.
Katika
mechi ya mzunguko wa kwanza iliyopigwa Oktoba 8, 2012 kwenye Uwanja wa Kaitaba
mjini Bukoba, Kagera Sugar iliibuka na ushindi wa bao 1-0 lililofungwa na Themi
Felix katika dakika ya 68.
Maana yake, Yanga leo itakuwa inapambana kupata pointi
hizo muhimu lakini kulipa kisasi pia.
0 COMMENTS:
Post a Comment